< Ayubu 31 >
1 Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
Zawarłem przymierze ze swoimi oczami; jak mógłbym więc myśleć o pannie?
2 Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
Jaki bowiem byłby dział od Boga z góry? I jakie byłoby dziedzictwo od Wszechmocnego z wysoka?
3 Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
Czy zatracenie nie jest [przygotowane] dla niegodziwych i sroga pomsta dla czyniących nieprawość?
4 Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
Czyż on nie widzi moich dróg i nie liczy wszystkich moich kroków?
5 Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
Jeśli postępowałem kłamliwie, jeśli moja noga spieszyła się do oszustwa;
6 na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
To niech zważy mnie na wadze sprawiedliwej i niech Bóg pozna moją prawość.
7 Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
Jeśli moja noga zboczyła z drogi i moje serce poszło za moimi oczami, i jeśli jakaś zmaza przylgnęła do moich rąk;
8 na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
Wtedy niech ja sieję, a inny spożywa, niech moje latorośle będą wykorzenione.
9 Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
Jeśli moje serce uwiodła kobieta i jeśli czyhałem pod drzwiami swego bliźniego;
10 na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
To niech moja żona mieli innemu i niech inni się nad nią schylają.
11 Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
[Jest] to bowiem haniebny czyn, karygodna nieprawość;
12 Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
To jest ogień, który pożera aż do zatracenia i może wykorzenić cały mój dobytek.
13 Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
Jeśli zlekceważyłem sprawę swojego sługi albo swojej służącej, gdy wiedli spór ze mną;
14 kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
Co zrobię, gdy Bóg powstanie? Gdy mnie nawiedzi, co mu odpowiem?
15 Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
Czy ten, który mnie stworzył w łonie, nie stworzył też jego? Czy nie on jeden ukształtował nas w łonie?
16 kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
Jeśli odmówiłem prośbie ubogich i jeśli zasmuciłem oczy wdowy;
17 au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
Jeśli sam jadłem swoją kromkę [i] nie jadła z niej sierota;
18 kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
(Od swojej młodości bowiem wychowywałem ją jak ojciec, a od łona swojej matki prowadziłem [wdowę]);
19 ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
Jeśli widziałem ginącego z powodu braku ubrania albo biedaka bez okrycia;
20 ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
Jeśli jego biodra nie błogosławiły mi dlatego, że się zagrzał wełną moich owiec;
21 ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
Jeśli podniosłem rękę przeciwko sierocie, gdy widziałem w bramie swoją pomoc;
22 Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
Wtedy niech odpadnie mój bark od karku, a niech moje ramię wyjdzie ze stawu.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
Bałem się bowiem klęski od Boga, a przed jego majestatem nie mógłbym [się ostać].
24 Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
Jeśli pokładałem w złocie swoją nadzieję, a do czystego złota mówiłem: [Ty jesteś] moją ufnością;
25 na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
Jeśli radowałem się ze swojego wielkiego bogactwa i [tego], że moja ręka nabyła wiele;
26 Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
Jeśli patrzyłem na słońce, gdy świeciło, i na księżyc, gdy sunął wspaniale;
27 na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
A moje serce dało się uwieść potajemnie i moje usta całowały moją rękę;
28 hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
I to byłaby nieprawość karygodna, bo zaparłbym się Boga z wysoka.
29 Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
Jeśli cieszyłem się z upadku tego, który mnie nienawidzi, jeśli wyniosłem się, gdy mu się źle wiodło;
30 Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
(Nawet nie pozwoliłem zgrzeszyć swoim ustom, pragnąc przekleństwa na jego duszy);
31 Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
Czy ludzie z mojego namiotu nie mówili: Obyśmy mieli z jego mięsa! Nie możemy się najeść.
32 (hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
Obcy nie nocował na dworze, swoje drzwi otwierałem podróżnemu.
33 Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
Jeśli ukrywałem swoje przestępstwa jak Adam i chowałem w zanadrzu swoją nieprawość;
34 kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
Czy strach przed wielką zgrają albo pogarda bliskich przeraziły mnie, abym milczał i nie wychodził [za] drzwi?
35 Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
Obym miał kogoś, kto by mnie wysłuchał! Oto moja prośba, [aby] Wszechmogący odpowiedział mi i aby mój wróg napisał księgę.
36 Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
Czy nie nosiłbym jej na swoim ramieniu i nie przywiązałbym jej sobie [jak] koronę?
37 Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
Oznajmiłbym mu liczbę swoich kroków; zbliżyłbym się do niego jak książę.
38 Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
Jeśli moja ziemia wołała przeciwko mnie, jeśli razem z nią płakały jej bruzdy;
39 ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
Jeśli spożywałem z jej plonów bez zapłaty, jeśli jej właścicieli pozbawiłem życia;
40 ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.
Niech rosną ciernie zamiast pszenicy i sam kąkol zamiast jęczmienia. Skończyły się słowa Hioba.