< Ayubu 31 >
1 Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
covenant to cut: make(covenant) to/for eye my and what? to understand upon virgin
2 Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
and what? portion god from above and inheritance Almighty from height
3 Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
not calamity to/for unjust and misfortune to/for to work evil: wickedness
4 Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
not he/she/it to see: see way: conduct my and all step my to recount
5 Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
if to go: walk with vanity: false and to hasten upon deceit foot my
6 na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
to weigh me in/on/with balance righteousness and to know god integrity my
7 Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
if to stretch step my from [the] way: conduct and after eye my to go: went heart my and in/on/with palm my to cleave blemish
8 na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
to sow and another to eat and offspring my to uproot
9 Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
if to entice heart my upon woman and upon entrance neighbor my to ambush
10 na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
to grind to/for another woman: wife my and upon her to bow [emph?] another
11 Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
for (he/she/it *Q(K)*) wickedness (and he/she/it *Q(k)*) iniquity: crime judge
12 Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
for fire he/she/it till Abaddon to eat and in/on/with all produce my to uproot
13 Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
if to reject justice servant/slave my and maidservant my in/on/with strife their with me me
14 kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
and what? to make: do for to arise: rise God and for to reckon: visit what? to return: reply him
15 Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
not in/on/with belly: womb to make me to make him and to establish: make him in/on/with womb one
16 kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
if to withhold from pleasure poor and eye widow to end: expend
17 au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
and to eat morsel my to/for alone me and not to eat orphan from her
18 kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
for from youth my to magnify me like/as father and from belly: womb mother my to lead her
19 ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
if to see: see to perish from without clothing and nothing covering to/for needy
20 ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
if not to bless me (loin his *Q(K)*) and from fleece lamb my to warm
21 ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
if to wave upon orphan hand: power my for to see: see in/on/with gate help my
22 Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
shoulder my from shoulder [to] to fall: fall and arm my from branch: shoulder her to break
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
for dread to(wards) me calamity God and from elevation his not be able
24 Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
if to set: make gold loin my and to/for gold to say confidence my
25 na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
if to rejoice for many strength: rich my and for mighty to find hand my
26 Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
if to see: see light for to shine and moon precious to go: walk
27 na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
and to entice in/on/with secrecy heart my and to kiss hand my to/for lip my
28 hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
also he/she/it iniquity: crime judge for to deceive to/for God from above
29 Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
if to rejoice in/on/with disaster to hate me and to rouse for to find him bad: evil
30 Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
and not to give: allow to/for to sin palate my to/for to ask in/on/with oath soul: life his
31 Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
if not to say man tent my who? to give: allow from flesh his not to satisfy
32 (hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
in/on/with outside not to lodge sojourner door my to/for way to open
33 Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
if to cover like/as Adam transgression my to/for to hide in/on/with breast my iniquity: crime my
34 kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
for to tremble crowd many and contempt family to to be dismayed me and to silence: silent not to come out: come entrance
35 Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
who? to give: if only! to/for me to hear: hear to/for me look! mark my Almighty to answer me and scroll: document to write man strife my
36 Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
if: surely yes not upon shoulder my to lift: bear him to bind him crown to/for me
37 Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
number step my to tell him like leader to present: come him
38 Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
if upon me land: soil my to cry out and unitedness furrow her to weep [emph?]
39 ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
if strength her to eat without silver: money and soul: life master her to breathe
40 ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.
underneath: instead wheat to come out: issue thistle and underneath: instead barley foul weed to finish word Job