< Ayubu 31 >

1 Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
A covenant I made to eyes my and what? will I look carefully on a virgin.
2 Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
And what? - [is] [the] portion of God above and [the] inheritance of [the] Almighty from high places.
3 Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
¿ Not [does] calamity [belong] to an evil-doer and misfortune to [those who] do wickedness.
4 Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
¿ Not he does he see ways my and all steps my does he count?
5 Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
If I have walked with falsehood and it has made haste to deceit foot my.
6 na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
Let him weigh me in balances of righteousness and let him acknowledge God integrity my.
7 Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
If it turned aside step my from the way and after eyes my it has gone heart my and to hands my it has stuck a blemish.
8 na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
Let me sow and another let him eat and produce my let them be rooted up.
9 Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
If it has been deceived heart my on a woman and at [the] doorway of neighbor my I have lain in wait.
10 na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
Let her grind for another wife my and over her let them bow down! others.
11 Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
For (that *Q(K)*) [is] wickedness (and that *Q(k)*) [is] iniquity judges.
12 Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
For [is] a fire that [which] to Abaddon it will devour and all produce my it will root up.
13 Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
If I rejected [the] cause of male servant my and female servant my in complaint their with me.
14 kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
And what? will I do if he will arise God and if he will visit what? will I respond to him.
15 Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
¿ Not in the belly [the one who] made me did he make him and did prepare us? he in the womb one.
16 kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
If I withheld any of [the] desire of poor [people] and [the] eyes of a widow I caused to fail.
17 au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
And I may eat morsel of bread my to alone me and not he ate a fatherless one some of it.
18 kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
For since youth my he grew up with me like a father and from [the] womb of mother my I guided her.
19 ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
If I saw [one who] was perishing because not clothing and not covering [belonged] to the needy [person].
20 ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
If not they blessed me (loins his *Q(K)*) and from [the] fleece of lambs my he warmed himself.
21 ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
If I brandished on a fatherless one hand my for I saw in the gate help my.
22 Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
Shoulder my from its shoulder let it fall and arm my from arm its let it be broken.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
For [was] a fear to me calamity of God and from majesty his not I am able.
24 Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
If I have made gold confidence my and to pure gold I have said security my.
25 na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
If I rejoiced for [was] great wealth my and for much it had found hand my.
26 Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
If I saw a light that it shone and [the] moon splendid [was] going.
27 na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
And it was gullible in secrecy heart my and it kissed hand my mouth my.
28 hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
Also that [is] iniquity calling for judgment for I denied God above.
29 Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
If I rejoiced in [the] disaster of [one who] hated me and I excited myself if it had found him calamity.
30 Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
And not I have permitted to sin palate my by asking for by a curse life his.
31 Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
If not they have said [the] men of tent my who? will he give from meat his not [one who] is satisfied.
32 (hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
In the street not he passed [the] night a sojourner doors my to the path I opened.
33 Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
If I have concealed like Adam transgressions my by hiding in bosom my iniquity my.
34 kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
For I feared - a multitude great and [the] contempt of clans it caused to be dismayed me and I was silent not I went outside [the] door.
35 Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
Who? will he give [will belong] to me - [one who] listens to me here! mark my [the] Almighty let him answer me and a document [which] he had written [the] person of case my.
36 Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
If not on shoulder my I will carry it I will tie on it a crown to myself.
37 Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
[the] number of Steps my I will tell to him like a chief I will approach him.
38 Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
If on me land my it cried out and together furrows its they wept!
39 ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
If produce its I have eaten not money and [the] life of owners its I have caused to breathe out.
40 ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.
In place of wheat - let it come forth thorn[s] and in place of barley foul weed[s] they are finished [the] words of Job.

< Ayubu 31 >