< Ayubu 31 >
1 Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
Jeg sluttede en Pagt med mit Øje om ikke at se paa en Jomfru;
2 Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
hvad var ellers min Lod fra Gud hist oppe, den Arv, den Almægtige gav fra det høje?
3 Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
Har ikke den lovløse Vanheld i Vente, Udaadsmændene Modgang?
4 Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
Ser han ej mine Veje og tæller alle mine Skridt?
5 Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
Har jeg holdt til med Løgn, og hasted min Fod til Svig —
6 na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
paa Rettens Vægtskaal veje han mig, saa Gud kan kende min Uskyld —
7 Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
er mit Skridt bøjet af fra Vejen, og har mit Hjerte fulgt mine Øjne, hang noget ved mine Hænder,
8 na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
da gid jeg maa saa og en anden fortære, og hvad jeg planted, oprykkes med Rode!
9 Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
Blev jeg en Daare paa Grund af en Kvinde, og har jeg luret ved Næstens Dør,
10 na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
saa dreje min Hustru Kværn for en anden, og andre bøje sig over hende!
11 Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
Thi sligt var Skændselsdaad, Brøde, der drages for Retten,
12 Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
ja, Ild, der æder til Afgrunden og sætter hele min Høst i Brand!
13 Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
Har jeg ringeagtet min Træls og min Trælkvindes Ret, naar de trættede med mig,
14 kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
hvad skulde jeg da gøre, naar Gud stod op, hvad skulde jeg svare, naar han saa efter?
15 Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
Har ikke min Skaber skabt ham i Moders Skød, har en og samme ej dannet os begge i Moders Liv?
16 kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
Har jeg afslaaet ringes Ønske, ladet Enkens Øjne vansmægte,
17 au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
var jeg ene om at spise mit Brød, har den faderløse ej spist deraf —
18 kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
nej, fra Barnsben fostred jeg ham som en Fader, jeg ledede hende fra min Moders Skød.
19 ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
Har jeg set en Stakkel blottet for Klæder, en fattig savne et Tæppe —
20 ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
visselig nej, hans Hofter velsigned mig, naar han varmed sig i Uld af mine Lam.
21 ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
Har jeg løftet min Baand mod en faderløs, fordi jeg var vis paa Medhold i Retten,
22 Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
saa falde min Skulder fra Nakken, saa rykkes min Arm af Led!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
Thi Guds Rædsel var kommet over mig, og naar han rejste sig, magted jeg intet!
24 Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
Har jeg slaaet min Lid til Guld, kaldt det rene Guld min Fortrøstning,
25 na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
var det min Glæde, at Rigdommen voksed, og at min Haand fik sanket saa meget,
26 Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
saa jeg, hvorledes Sollyset straaled, eller den herligt skridende Maane,
27 na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
og lod mit Hjerte sig daare i Løn, saa jeg hylded dem med Kys paa min Haand —
28 hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
ogsaa det var Brøde, der drages for Retten, thi da fornægted jeg Gud hist oppe.
29 Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
Var min Avindsmands Fald min Glæd jubled jeg, naar han ramtes af Vanheld —
30 Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
nej, jeg tillod ikke min Gane at synde, saa jeg bandende kræved hans Sjæl.
31 Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
Har min Husfælle ej maattet sige: »Hvem mættedes ej af Kød fra hans Bord« —
32 (hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
nej, den fremmede laa ej ude om Natten, jeg aabned min Dør for Vandringsmænd.
33 Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
Har jeg skjult mine Synder, som Mennesker gør, saa jeg dulgte min Brøde i Brystet
34 kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
af Frygt for den store Hob, af Angst for Stamfrænders Ringeagt, saa jeg blev inden Døre i Stilhed! —
35 Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
Ak, var der dog en, der hørte paa mig! Her er mit Bomærke — lad den Almægtige svare! Havde jeg blot min Modparts Indlæg!
36 Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
Sandelig, tog jeg det paa min Skulder, kransed mit Hoved dermed som en Krone,
37 Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
svared ham for hvert eneste Skridt og mødte ham som en Fyrste.
38 Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
Har min Mark maattet skrige over mig og alle Furerne græde,
39 ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
har jeg tæret dens Kraft uden Vederlag, udslukt dens Ejeres Liv,
40 ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.
saa gro der Tjørn for Hvede og Ukrudt i Stedet for Byg! Her ender Jobs Ord.