< Ayubu 30 >
1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
Mais maintenant je suis tourné en ridicule par des hommes plus jeunes que moi, dont autrefois je n’aurais pas daigné mettre les pères avec les chiens de mon troupeau;
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Dont je comptais pour rien la force de la main, et qui me paraissaient même indignes de la vie;
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
Qui desséchés par la détresse et la faim, rongeaient dans un désert ce qu’ils pouvaient y trouver, défigurés par le malheur et la misère;
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Qui mangeaient des herbes et des écorces d’arbres, et dont la racine des genévriers était la nourriture;
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
Qui allaient les enlever dans les vallées, et qui, en ayant trouvé quelqu’une, y accouraient en criant;
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
Qui habitaient dans des déserts auprès des torrents, dans les cavernes de la terre, ou sur le gravier;
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
Qui au milieu de choses semblables se livraient à la joie, et mettaient leurs délices à être sous des ronces.
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
Fils de pères insensés et vils, et qui ne paraissent nullement sur la terre.
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
Maintenant je suis devenu le sujet de leurs chansons, et je suis passé parmi eux en proverbe.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
Ils m’ont en horreur, et ils fuient loin de moi, et ils n’ont pas honte de cracher sur ma face.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
Car Dieu a ouvert son carquois, et il m’a abattu, et il a mis un frein à ma bouche.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
À ma droite, quand j’ai commencé à paraître, mes maux se sont soudain élevés; ils ont renversé mes pieds, et m’ont foulé dans leurs sentiers comme sous des flots.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
Ils ont détruit mes chemins, ils m’ont dressé des pièges et ils ont prévalu, et il n’y a eu personne qui me portât secours.
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
Comme par la brèche d’un mur et par une porte ouverte ils ont fondu sur moi, et ils ont accouru pour m’accabler dans ma misère.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
J’ai été réduit au néant; comme le vent, vous avez emporté l’objet de mes désirs, et comme un nuage, a passé mon bonheur.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
Aussi maintenant mon âme se flétrit en moi-même, et des jours d’affliction ont pris possession de moi.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
Pendant la nuit mes os sont transpercés de douleurs; et ceux qui me dévorent ne dorment pas.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
Leur multitude consume mon vêtement, et ils m’ont couvert comme d’un capuchon de tunique.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
Je suis devenu comme la boue, et je suis semblable à la braise et à la cendre.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
Je crie vers vous, et vous ne m’exaucez pas; je me liens devant vous, et vous ne me regardez pas.
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
Vous êtes changé et devenu cruel envers moi; et c’est avec la dureté de votre main que vous me combattez.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
Vous m’avez élevé, et me posant comme sur le vent, vous m’avez brisé entièrement.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
Je sais que vous me livrerez à la mort, où est marquée la maison de tous les vivants.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Cependant ce n’est pas pour leur ruine que vous étendez votre main; car s’ils tombent, vous les sauvez.
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
Je pleurais autrefois sur celui qui était affligé, et mon âme était compatissante pour le pauvre.
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
J’attendais des biens, et il m’est venu des maux; j’espérais la lumière, et des ténèbres se sont répandues autour de moi.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
Un feu ardent n’a cessé de brûler dans mes entrailles; des jours d’affliction m’ont prévenu.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
Je marchais triste, sans fureur; me levant, je poussais des cris au milieu de la foule.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
J’ai été frère des dragons et compagnon des autruches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
Ma peau est devenue noire sur moi, et mes os se sont desséchés dans une ardeur brûlante.
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
Ma harpe s’est changée en plainte lugubre, et mon orgue en voix de pleureurs.