< Ayubu 30 >

1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
Et maintenant, je suis la risée d’hommes plus jeunes que moi, dont je n’aurais pas daigné mettre les pères parmi les chiens de mon troupeau.
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Qu’aurais-je fait de la force de leurs bras? Ils sont privés de toute vigueur.
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
Desséchés par la misère et la faim, ils broutent le désert, un sol depuis longtemps aride et désolé.
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Ils cueillent sur les buissons des bourgeons amers, ils n’ont pour pain que la racine des genêts.
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
On les écarte de la société des hommes, on crie après eux comme après le voleur.
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
Ils habitent dans d’affreuses vallées, dans les cavernes de la terre et les rochers.
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
On entend leurs cris sauvages parmi les broussailles, ils se couchent ensemble sous les ronces:
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
gens insensés, race sans nom, bannis avec mépris de la terre habitée!
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
Et maintenant je suis l’objet de leurs chansons, je suis en butte à leurs propos.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
Ils ont horreur de moi, ils me fuient, ils ne détournent pas leur crachat de mon visage.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
Ils se donnent libre carrière pour m’outrager, ils rejettent tout frein devant moi.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
Des misérables se lèvent à ma droite, ils cherchent à ébranler mes pieds, ils frayent jusqu’à moi leurs routes meurtrières.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
Ils ont bouleversé mes sentiers, ils travaillent à ma ruine, eux à qui personne ne porterait secours.
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
Ils fondent sur moi, comme par une large brèche, ils se précipitent parmi les décombres.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
Les terreurs m’assiègent, ma prospérité est emportée comme un souffle, mon bonheur a passé comme un nuage.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
Et maintenant, mon âme s’épanche en moi, les jours d’affliction m’ont saisi.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
La nuit perce mes os, les consume, le mal qui me ronge ne dort pas.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
Par sa violence, mon vêtement a perdu sa forme, il me serre comme une tunique.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
Dieu m’a jeté dans la fange, je suis comme la poussière et la cendre.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
Je crie vers toi, et tu ne me réponds pas; je me tiens debout, et tu me regardes avec indifférence.
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
Tu deviens cruel à mon égard, tu m’attaques avec toute la force de ton bras.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
Tu m’enlèves, tu me fais voler au gré du vent, et tu m’anéantis dans le fracas de la tempête.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
Car, je le sais, tu me mènes à la mort, au rendez-vous de tous les vivants.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Cependant celui qui va périr n’étendra-t-il pas les mains et, dans sa détresse, ne poussera-t-il pas un cri?
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
N’avais-je pas des larmes pour l’infortuné? Mon cœur ne s’est-il pas attendri sur l’indigent?
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
J’attendais le bonheur, et le malheur est arrivé; j’espérais la lumière, et les ténèbres sont venues.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
Mes entrailles bouillonnent sans relâche, les jours d’affliction ont fondu sur moi.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
Je marche dans le deuil, sans soleil; si je me lève dans l’assemblée, c’est pour pousser des cris.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
Je suis devenu le frère des chacals, le compagnon des filles de l’autruche.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
Ma peau livide tombe en lambeaux, mes os sont brûlés par un feu intérieur.
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
Ma cithare ne rend plus que des accords lugubres, mon chalumeau que des sons plaintifs.

< Ayubu 30 >