< Ayubu 30 >

1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
But now they that are younger than I hold me in derision, whose fathers I would have disdained to set with the dogs of my flock.
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Yea, to what might the strength of their hands profit me, in whom old age had perished?
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
For want and famine they were solitary; fleeing into the wilderness in former time desolate and waste.
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Who cut up mallows by the bushes, and juniper roots for their food.
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
They were driven forth from among men, (they cried after them as after a thief; )
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
To dwell in the clefts of the valleys, in caves of the earth, and in the rocks.
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
Among the bushes they brayed; under the nettles they were gathered together.
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
They were children of fools, yea, children of base men: they were viler than the earth.
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
And now I am their song, yea, I am their byword.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
They abhor me, they flee far from me, and spare not to spit in my face.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
Because he hath loosed my cord, and afflicted me, they have also let loose the bridle before me.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
Upon my right hand rise the youth; they push away my feet, and they raise up against me the ways of their destruction.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
They mar my path, they set forward my calamity, they have no helper.
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
They came upon me as a wide breaking in of waters: in the desolation they rolled themselves upon me.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
Terrors are turned upon me: they pursue my soul as the wind: and my welfare passeth away as a cloud.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
And now my soul is poured out upon me; the days of affliction have taken hold upon me.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
My bones are pierced in me in the night season: and my sinews take no rest.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
By the great force of my disease is my garment changed: it bindeth me about as the collar of my coat.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
He hath cast me into the mire, and I have become like dust and ashes.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
I cry to thee, and thou dost not hear me: I stand up, and thou regardest me not.
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
Thou hast become cruel to me: with thy strong hand thou opposest thyself against me.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
Thou liftest me up to the wind; thou causest me to ride upon it, and dissolvest my substance.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
For I know that thou wilt bring me to death, and to the house appointed for all living.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Yet he will not stretch out his hand to the grave, though they cry in his destruction.
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
Did not I weep for him that was in trouble? was not my soul grieved for the poor?
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
When I looked for good, then evil came: and when I waited for light, there came darkness.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
My bowels boiled, and rested not: the days of affliction came upon me.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
I went mourning without the sun: I stood up, and I cried in the congregation.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
I am a brother to dragons, and a companion to owls.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
My skin is black upon me, and my bones are burned with heat.
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
My harp also is turned to mourning, and my organ into the voice of them that weep.

< Ayubu 30 >