< Ayubu 30 >
1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
But now the youngest have laughed me to scorn, now they reprove me in [their] turn, whose fathers I set at nothing; whom I did not deem worthy [to be with] my shepherd dogs.
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Yes, why had I the strength of their hands? for them the full term [of life] was lost.
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
[One is] childless in lack and famine, [such as] they that fled but lately the distress and misery of drought.
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Who compass the salt places on the sounding [shore], who had salt [herbs] for their food, and were dishonourable and of no repute, in lack of every good thing; who also ate roots of trees by reason of great hunger.
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
Thieves have risen up against me,
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
whose houses were the caves of the rocks, who lived under the wild shrubs.
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
They will cry out amongst the rustling [bushes].
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
[They are] sons of fools and vile men, [whose] name and glory [are] quenched from off the earth.
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
But now I am their music, and they have me for a byword.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
And they stood aloof and abhorred me, and spared not to spit in my face.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
For he has opened his quiver and afflicted me: they also have cast off the restraint of my presence.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
They have risen up against [me] on the right hand of [their] offspring; they have stretched out their foot, and directed against me the ways of their destruction.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
My paths are ruined; for they have stripped off my raiment: he has shot at me with his weapons.
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
And he has pleaded against me as he will: I am overwhelmed with pains.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
My pains return upon [me]; my hope is gone like the wind, and my safety as a cloud.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
Even now my life shall be poured forth upon me; and days of anguish seize me.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
And by night my bones are confounded; and my sinews are relaxed.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
With great force [my disease] has taken hold of my garment: it has compassed me as the collar of my coat.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
And you have counted me as clay; my portion in dust and ashes.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
And I have cried to you, but you hear me not: but they stood still, and observed me.
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
They attacked me also without mercy: you have scourged me with a strong hand.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
And you have put me to grief, and have cast me away from safety.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
For I know that death will destroy me: for the earth is the house [appointed] for every mortal.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Oh then that I might lay hands upon myself, or at least ask another, and he should do this for me.
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
Yet I wept over every helpless man; I groaned when I saw a man in distress.
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
But I, when I waited for good things, behold, days of evils came the more upon me.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
My belly boiled, and would not cease: the days of poverty prevented me.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
I went mourning without restraint: and I have stood and cried out in the assembly.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
I am become a brother of monsters, and a companion of ostriches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
And my skin has been greatly blackened, and my bones are burnt with heat.
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
My harp also has been turned into mourning, and my song into my weeping.