< Ayubu 3 >
1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
Après cela, Job ouvrit la bouche et maudit le jour de sa naissance.
Il prit la parole et dit:
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
Périsse le jour où je suis né, Et la nuit qui dit: Un enfant mâle est conçu!
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
Ce jour! Qu’il se change en ténèbres, Que Dieu n’en ait point souci dans le ciel, Et que la lumière ne rayonne plus sur lui!
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Que l’obscurité et l’ombre de la mort s’en emparent, Que des nuées établissent leur demeure au-dessus de lui, Et que de noirs phénomènes l’épouvantent!
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
Cette nuit! Que les ténèbres en fassent leur proie, Qu’elle disparaisse de l’année, Qu’elle ne soit plus comptée parmi les mois!
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Que cette nuit devienne stérile, Que l’allégresse en soit bannie!
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Qu’elle soit maudite par ceux qui maudissent les jours, Par ceux qui savent exciter le léviathan!
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Que les étoiles de son crépuscule s’obscurcissent, Qu’elle attende en vain la lumière, Et qu’elle ne voie point les paupières de l’aurore!
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
Car elle n’a pas fermé le sein qui me conçut, Ni dérobé la souffrance à mes regards.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Pourquoi ne suis-je pas mort dans le ventre de ma mère? Pourquoi n’ai-je pas expiré au sortir de ses entrailles?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Pourquoi ai-je trouvé des genoux pour me recevoir, Et des mamelles pour m’allaiter?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
Je serais couché maintenant, je serais tranquille, Je dormirais, je reposerais,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
Avec les rois et les grands de la terre, Qui se bâtirent des mausolées,
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Avec les princes qui avaient de l’or, Et qui remplirent d’argent leurs demeures.
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
Ou je n’existerais pas, je serais comme un avorton caché, Comme des enfants qui n’ont pas vu la lumière.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
Là ne s’agitent plus les méchants, Et là se reposent ceux qui sont fatigués et sans force;
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
Les captifs sont tous en paix, Ils n’entendent pas la voix de l’oppresseur;
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
Le petit et le grand sont là, Et l’esclave n’est plus soumis à son maître.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Pourquoi donne-t-il la lumière à celui qui souffre, Et la vie à ceux qui ont l’amertume dans l’âme,
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Qui espèrent en vain la mort, Et qui la convoitent plus qu’un trésor,
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
Qui seraient transportés de joie Et saisis d’allégresse, s’ils trouvaient le tombeau?
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
A l’homme qui ne sait où aller, Et que Dieu cerne de toutes parts?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
Mes soupirs sont ma nourriture, Et mes cris se répandent comme l’eau.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
Ce que je crains, c’est ce qui m’arrive; Ce que je redoute, c’est ce qui m’atteint.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
Je n’ai ni tranquillité, ni paix, ni repos, Et le trouble s’est emparé de moi.