< Ayubu 3 >
1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
Finally, Job spoke, and he cursed the day that he was born.
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
“I wish that the day when I was born could be eradicated, and also the night when I was conceived.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
I wish that the day when I was born would have been covered in darkness. I wish that God who is in heaven [MTY] would have forgotten about that day, and that the sun would not have shone on it.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
I wish that thick/intense darkness would have filled that day, and that a black cloud would have come over it and blotted out all light and caused people to be terrified.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
I wish that the night when I was conceived would be erased from the calendar, with the result that it would never again appear as one night in any month, and that it would not be included in any calendar.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
I wish that no child would again be conceived on that night of the month [MET], and that no one would again be happy on that night.
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
I want those people who (curse/put evil spells on) days—those who know how to arouse/awaken the great sea monster—to curse that day.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
I wish that the stars that shone early in the morning on that day [after I was conceived] will not shine again. I want those stars to have wished in vain for light to shine; and that they would not have shone on that day.
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
[That was an evil day] because my mother was able to conceive; instead, I was born, and I have now experienced all these terrible things.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
“I wish that I had died [RHQ] when I was born— at the time I emerged from my mother’s womb.
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
I wish that my mother had not [RHQ] allowed me to live. I wish that she had not nursed me.
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
If I had died at the time when I was born, I would be asleep, resting peacefully [in the place where the dead people are].
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
I would be resting with kings whose [beautiful palaces] that they built are now in ruins (OR, who rebuilt [palaces] that had previously been destroyed), and I would be resting with their officials [who have also died].
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
I would be resting with princes who were wealthy, whose palaces were filled with gold and silver.
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
I wish that I had been buried like a child who died in its mother’s womb and never lived to see the light.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
After wicked people die, they do not cause any more troubles; those who are very tired now will rest.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
Those who were in prison rest peacefully [after they die]; they no longer have slave-drivers who curse them.
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
Rich people and poor people are alike after they die, and those who were slaves are no longer controlled by their masters.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
(“Why does God allow those who are suffering greatly [like me] to continue to remain alive?/I do not understand why God allows those who are suffering greatly [like me] to continue to remain alive.) [RHQ] Why does he allow those who are very miserable/distressed to keep living [RHQ]?
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
They long/want to die, but they do not die. They desire to die more than people desire to find a hidden treasure.
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
When they finally die and are buried, they are very happy.
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
Those who do not know where they are [eventually] going when they die [RHQ], people whom God has forced [MET] to continue to live in misery, (it is not right that they continue to live./why do they continue to live?) [RHQ]
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
I continually cry very much; as a result, I cannot eat; and I can never stop groaning.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
Things that I always worried might happen to me, have happened to me; things that I always dreaded have happened to me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
Now I have no peace [in my inner being], I have no peace; I cannot rest; instead, I have only troubles.”