< Ayubu 3 >

1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
After thus he opened Job mouth his and he cursed day his.
2 Akasema,
And he answered Job and he said.
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
Let it perish [the] day [which] I was born on it and the night [which] it said he has been conceived a man.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
The day that let it be darkness may not he care for it God above and may not it shine forth on it daylight.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Let them reclaim it darkness and deep darkness let it settle down over it cloud let them terrify it [the] darkness of day.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
The night that let it take it darkness may not it rejoice among [the] days of [the] year in [the] number of [the] months may not it come.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
There! the night that let it be barren may not it come a cry of joy in it.
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Let them curse it cursers of a day the [ones] ready to rouse Leviathan.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Let them grow dark [the] stars of twilight its let it wait for light and not and may not it look on [the] eyelids of dawn.
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
For not it shut [the] doors of womb my and it hid trouble from eyes my.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Why? not from [the] womb did I die from [the] belly I came forth and I may expire?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Why? did they receive me knees and why? breasts that I will suckle.
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
For now I lay down and I may be at peace I slept then - it is at rest to me.
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
With kings and counselors of [the] earth the [ones who] rebuilt ruins for themselves.
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Or with princes [whom] gold [belonged] to them those [who] filled houses their silver.
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
Or like a miscarriage hidden not was I? like children [who] not they have seen light.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
There wicked [people] they cease turmoil and there they rest weary [ones] of strength.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
Together prisoners they are at ease not they hear [the] voice of a taskmaster.
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
Small and great [is] there he and a slave [is] free from master his.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Why? does someone give to a sufferer light and life to [people] bitter of soul.
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Those [who] long for death and there not [is] it and they dug for it more than hidden treasures.
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
The joyful [people] to rejoicing they exult if they find [the] grave.
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
To a man whom way his it is hidden and he has made inaccessible God behind him.
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
If before food my groaning my it comes and they poured forth like water cries of distress my.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
For a fear I feared and it came to me and [that] which I dreaded it came to me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
Not I am at ease - and not I am at peace and not I am at rest and it has come turmoil.

< Ayubu 3 >