< Ayubu 3 >

1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
After this Job has opened his mouth, and reviles his day.
2 Akasema,
And Job answers and says:
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
“Let the day perish in which I am born, And the night that has said: A man-child has been conceived.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
That day—let it be darkness, Do not let God require it from above, Nor let light shine on it.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Let darkness and death-shade redeem it, Let a cloud dwell on it, Let them terrify it as the most bitter of days.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
That night—let thick darkness take it, Let it not be united to days of the year, Let it not come into the number of months.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Behold! That night—let it be barren, Let no singing come into it.
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Let the cursers of day mark it, Who are ready to wake up Leviathan.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Let the stars of its twilight be dark, Let it wait for light, and there is none, And let it not look on the eyelids of the dawn.
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
Because it has not shut the doors Of the womb that was mine! And hide misery from my eyes.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Why do I not die from the womb? I have come forth from the belly and gasp!
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Why have knees been before me? And what [are] breasts, that I suck?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
For now, I have lain down, and am quiet, I have slept—then there is rest to me,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
With kings and counselors of earth, These building ruins for themselves.
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Or with princes—they have gold, They are filling their houses [with] silver.
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
(Or I am not as a hidden abortion, As infants—they have not seen light.)
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
There the wicked have ceased troubling, And there the wearied rest in power.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
Together prisoners have been at ease, They have not heard the voice of an exactor,
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
Small and great [are] the same there. And a servant [is] free from his lord.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Why does He give light to the miserable, and life to the bitter soul?
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Who are waiting for death, and it is not, And they seek it above hid treasures.
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
Who are glad—to joy, They rejoice when they find a grave.
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
To a man whose way has been hidden, And whom God shuts up?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
For before my food, my sighing comes, And my roarings [are] poured out as waters.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
For I feared a fear and it meets me, And what I was afraid of comes to me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
I was not safe—nor was I quiet—Nor was I at rest—and trouble comes!”

< Ayubu 3 >