< Ayubu 3 >
1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
After this, Job opened his mouth and cursed his day.
And Job answered and said,
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
Let the day perish in which I was born, and the night that said, There is a man child conceived.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
That day — let it be darkness, let not God care for it from above, neither let light shine upon it:
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Let darkness and the shadow of death claim it; let clouds dwell upon it; let darkeners of the day terrify it.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
That night — let gloom seize upon it; let it not rejoice among the days of the year; let it not come into the number of the months.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Behold, let that night be barren; let no joyful sound come therein;
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Let them curse it that curse the day, who are ready to rouse Leviathan;
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Let the stars of its twilight be dark; let it wait for light, and have none, neither let it see the eyelids of the dawn:
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
Because it shut not up the doors of the womb that bore me, and hid not trouble from mine eyes.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Wherefore did I not die from the womb, — come forth from the belly and expire?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Why did the knees meet me? and wherefore the breasts, that I should suck?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
For now should I have lain down and been quiet; I should have slept: then had I been at rest,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
With kings and counsellors of the earth, who build desolate places for themselves,
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Or with princes who had gold, who filled their houses with silver;
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
Or as a hidden untimely birth I had not been; as infants that have not seen the light.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
There the wicked cease from troubling; and there the wearied are at rest.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
The prisoners together are at ease; they hear not the voice of the taskmaster.
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
The small and great are there, and the bondman freed from his master.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Wherefore is light given to him that is in trouble, and life to those bitter of soul,
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Who long for death, and it [cometh] not, and dig for it more than for hidden treasures;
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
Who rejoice even exultingly and are glad when they find the grave? —
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
To the man whose way is hidden, and whom God hath hedged in?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
For my sighing cometh before my bread, and my groanings are poured out like the waters.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
For I feared a fear, and it hath come upon me, and that which I dreaded hath come to me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
I was not in safety, neither had I quietness, neither was I at rest, and trouble came.