< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na kusema,
Und Hiob hub abermal an seine Sprüche und sprach:
2 Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
O daß ich wäre wie in den vorigen Monden, in den Tagen, da mich Gott behütete,
3 taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
da seine Leuchte über meinem Haupte schien, und ich bei seinem Licht in der Finsternis ging;
4 Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
wie ich war zur Zeit meiner Jugend, da Gottes Geheimnis über meiner Hütte war;
5 wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
da der Allmächtige noch mit mir war und meine Kinder um mich her;
6 wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
da ich meine Tritte wusch in Butter, und die Felsen mir Ölbäche gossen;
7 Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
da ich ausging zum Tor in der Stadt und ließ meinen Stuhl auf der Gasse bereiten;
8 vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
da mich die Jungen sahen und sich versteckten, und die Alten vor mir aufstunden;
9 Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
da die Obersten aufhöreten zu reden, und legten ihre Hand auf ihren Mund;
10 Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
da die Stimme der Fürsten sich verkroch, und ihre Zunge an ihrem Gaumen klebte.
11 Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
Denn welches Ohr mich hörete, der preisete mich selig, und welches Auge mich sah, der rühmte mich.
12 kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
Denn ich errettete den Armen, der da schrie, und den Waisen, der keinen Helfer hatte.
13 Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
Der Segen des, der verderben sollte, kam über mich; und ich erfreuete das Herz der Witwe.
14 Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
Gerechtigkeit war mein Kleid, das ich anzog wie einen Rock; und mein Recht war mein fürstlicher Hut.
15 Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
Ich war des Blinden Auge und des Lahmen Füße.
16 Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
Ich war ein Vater der Armen; und welche Sache ich nicht wußte, die erforschete ich.
17 Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
Ich zerbrach die Backenzähne des Ungerechten und riß den Raub aus seinen Zähnen.
18 Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
Ich gedachte: Ich will in meinem Nest ersterben und meiner Tage viel machen wie Sand.
19 Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
Meine Saat ging auf am Wasser; und der Tau blieb über meiner Ernte.
20 Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
Meine HERRLIchkeit erneuerte sich immer an mir; und mein Bogen besserte sich in meiner Hand.
21 Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
Man hörete mir zu, und schwiegen und warteten auf meinen Rat.
22 Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
Nach meinen Worten redete niemand mehr; und meine Rede troff auf sie.
23 Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
Sie warteten auf mich wie auf den Regen und sperreten ihren Mund auf als nach dem Abendregen.
24 Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
Wenn ich sie anlachte, wurden sie nicht zu kühn darauf, und das Licht meines Angesichts machte mich nicht geringer.
25 Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.
Wenn ich zu ihrem Geschäfte wollte kommen, so mußte ich obenan sitzen und wohnete wie ein König unter Kriegsknechten, da ich tröstete, die Leid trugen.