< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na kusema,
Et Job continuant, reprit son discours sentencieux, et dit:
2 Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
Oh! qui me ferait être comme j'étais autrefois, comme j'étais en ces jours où Dieu me gardait.
3 taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
Quand il faisait luire sa lampe sur ma tête, et quand je marchais parmi les ténèbres, [éclairé] par sa lumière.
4 Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
Comme j'étais aux jours de mon automne, lorsque le secret de Dieu était dans ma tente.
5 wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
Quand le Tout-puissant était encore avec moi, et mes gens autour de moi.
6 wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
Quand je lavais mes pas dans le beurre, et que des ruisseaux d'huile découlaient pour moi du rocher.
7 Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
Quand je sortais vers la porte passant par la ville, et que je me faisais préparer un siège dans la place,
8 vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
Les jeunes gens me voyant se cachaient, les vieillards se levaient, et se tenaient debout.
9 Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
Les principaux s'abstenaient de parler, et mettaient la main sur leur bouche.
10 Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
Les Conducteurs retenaient leur voix, et leur langue était attachée à leur palais.
11 Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
L'oreille qui m'entendait, disait que j'étais bienheureux, et l'œil qui me voyait, déposait en ma faveur.
12 kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
Car je délivrais l'affligé qui criait, et l'orphelin qui n'avait personne pour le secourir.
13 Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
La bénédiction de celui qui s'en allait périr, venait sur moi, et je faisais que le cœur de la veuve chantait de joie.
14 Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
J'étais revêtu de la justice, elle me servait de vêtement, et mon équité m'était comme un manteau, et [comme] une tiare.
15 Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
Je servais d'œil à l'aveugle, et de pieds au boiteux.
16 Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
J'étais le père des pauvres, et je m'informais diligemment de la cause qui ne m'était point connue.
17 Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
Je cassais les grosses dents de l'injuste, et je lui arrachais la proie d'entre ses dents.
18 Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
C'est pourquoi je disais: Je mourrai dans mon lit, et je multiplierai mes jours comme les grains de sable.
19 Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
Ma racine était ouverte aux eaux, et la rosée demeurait toute la nuit sur mes branches.
20 Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
Ma gloire se renouvelait en moi, et mon arc était renforcé en ma main.
21 Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
On m'écoutait, et on attendait [que j'eusse parlé]; et lorsque j'avais dit mon avis, on se tenait dans le silence.
22 Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
Ils ne répliquaient rien après ce que je disais, et ma parole se répandait sur eux [comme une rosée].
23 Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
Ils m'attendaient comme on attend la pluie; ils ouvraient leur bouche, comme après la pluie de la dernière saison.
24 Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
Riais-je avec eux? ils ne le croyaient point; et ils ne faisaient point disparaître la sérénité de mon visage.
25 Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.
Voulais-je aller avec eux? j'étais assis au haut bout, j'étais entr'eux comme un Roi dans son armée, et comme un homme qui console les affligés.

< Ayubu 29 >