< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na kusema,
So Iob proceeded and continued his parable, saying,
2 Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
Oh that I were as in times past, when God preserued me!
3 taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
When his light shined vpon mine head: and when by his light I walked thorowe the darkenesse,
4 Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
As I was in the dayes of my youth: when Gods prouidence was vpon my tabernacle:
5 wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
When the almightie was yet with me, and my children round about me.
6 wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
When I washed my pathes with butter, and when the rocke powred me out riuers of oyle:
7 Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
When I went out to the gate, euen to the iudgement seat, and when I caused them to prepare my seate in the streete.
8 vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
The yong men saw me, and hid themselues, and the aged arose, and stood vp.
9 Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
The princes stayed talke, and layde their hand on their mouth.
10 Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
The voyce of princes was hidde, and their tongue cleaued to the roofe of their mouth.
11 Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
And when the eare heard me, it blessed me: and when the eye sawe me, it gaue witnesse to me.
12 kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
For I deliuered the poore that cryed, and the fatherlesse, and him that had none to helpe him.
13 Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
The blessing of him that was ready to perish, came vpon me, and I caused the widowes heart to reioyce.
14 Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
I put on iustice, and it couered me: my iudgement was as a robe, and a crowne.
15 Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
I was the eyes to the blinde, and I was the feete to the lame.
16 Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
I was a father vnto the poore, and when I knewe not the cause, I sought it out diligently.
17 Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
I brake also the chawes of the vnrighteous man, and pluckt the praye out of his teeth.
18 Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
Then I sayde, I shall die in my nest, and I shall multiplie my dayes as the sand.
19 Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
For my roote is spread out by the water, and the dewe shall lye vpon my branche.
20 Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
My glory shall renue towarde me, and my bowe shall be restored in mine hand.
21 Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
Vnto me men gaue eare, and wayted, and helde their tongue at my counsell.
22 Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
After my wordes they replied not, and my talke dropped vpon them.
23 Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
And they wayted for me, as for the raine, and they opened their mouth as for the latter rayne.
24 Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
If I laughed on them, they beleeued it not: neither did they cause the light of my countenance to fall.
25 Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.
I appoynted out their way, and did sit as chiefe, and dwelt as a King in the army, and like him that comforteth the mourners.