< Ayubu 28 >

1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
Denn für das Silber gibt es einen Fundort, und eine Stätte für das Gold, das man läutert.
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Eisen wird hervorgeholt aus der Erde, und Gestein schmelzt man zu Kupfer.
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
Er hat der Finsternis ein Ende gesetzt, und durchforscht bis zur äußersten Grenze das Gestein der Finsternis und des Todesschattens.
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
Er bricht einen Schacht fern von dem Wohnenden; die von dem Fuße Vergessenen hangen hinab, fern von den Menschen schweben sie.
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
Die Erde, aus ihr kommt Brot hervor, und ihr Unteres wird zerwühlt wie vom Feuer.
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
Ihr Gestein ist der Sitz des Saphirs, und Goldstufen sind darin.
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
Ein Pfad, den der Raubvogel nicht kennt, und den das Auge des Habichts nicht erblickt hat;
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
den die wilden Tiere nicht betreten, über den der Löwe nicht hingeschritten ist.
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
Er legt seine Hand an das harte Gestein, wühlt die Berge um von der Wurzel aus.
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
Kanäle haut er durch die Felsen, und allerlei Köstliches sieht sein Auge.
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
Er dämmt Flüsse ein, daß sie nicht durchsickern, und Verborgenes zieht er hervor an das Licht.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Aber die Weisheit, wo wird sie erlangt? Und welches ist die Stätte des Verstandes?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Kein Mensch kennt ihren Wert, und im Lande der Lebendigen wird sie nicht gefunden.
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
Die Tiefe spricht: Sie ist nicht in mir, und das Meer spricht: Sie ist nicht bei mir.
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
Geläutertes Gold kann nicht für sie gegeben, und Silber nicht dargewogen werden als ihr Kaufpreis.
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
Sie wird nicht aufgewogen mit Gold von Ophir, mit kostbarem Onyx und Saphir.
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Gold und Glas kann man ihr nicht gleichstellen, noch sie eintauschen gegen ein Gerät von gediegenem Golde.
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
Korallen und Kristall kommen neben ihr nicht in Erwähnung; und der Besitz der Weisheit ist mehr wert als Perlen.
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
Nicht kann man ihr gleichstellen den Topas von Äthiopien; mit feinem Golde wird sie nicht aufgewogen.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Die Weisheit nun, woher kommt sie, und welches ist die Stätte des Verstandes?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Denn sie ist verborgen vor den Augen aller Lebendigen, und vor den Vögeln des Himmels ist sie verhüllt.
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
Der Abgrund und der Tod sagen: Mit unseren Ohren haben wir ein Gerücht von ihr gehört.
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
Gott versteht ihren Weg, und er kennt ihre Stätte.
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
Denn er schaut bis zu den Enden der Erde; unter dem ganzen Himmel sieht er.
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
Als er dem Winde ein Gewicht bestimmte, und die Wasser mit dem Maße abwog,
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
als er dem Regen ein Gesetz bestimmte und eine Bahn dem Donnerstrahl:
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
da sah er sie und tat sie kund, er setzte sie ein und durchforschte sie auch.
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
Und zu dem Menschen sprach er: Siehe, die Furcht des Herrn ist Weisheit, und vom Bösen weichen ist Verstand.

< Ayubu 28 >