< Ayubu 28 >

1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
Certes, il existe des mines pour l’argent et des gîtes pour 'l’or que l’on affine.
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Le fer est extrait du sol, et la roche, fondue, donne du cuivre.
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
Le mineur a posé des limites à l’obscurité; jusqu’aux extrêmes profondeurs il va chercher le minerai caché dans les ténèbres et l’ombre de la mort.
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
Il perce des tranchées à l’écart des habitations; ignoré du pied des passants, il est suspendu et ballotté loin des hommes.
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
La terre d’où sort le pain, ses entrailles sont bouleversées comme par le feu.
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
Ses pierres sont des nids de saphirs, et là s’offre au regard la poudre d’or.
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
On y arrive par un chemin que l’oiseau de proie ne connaît pas, que l’œil du vautour ne distingue point.
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
Les fauves altiers ne l’ont pas foulé, le lion ne l’a pas franchi.
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
Le mineur porte la main sur le granit, et il remue les montagnes jusqu’à leur racine.
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
Il perce des galeries à travers les roches, et son œil contemple les plus rares richesses.
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
Il aveugle les voies d’eau pour empêcher Ies infiltrations et amène au jour ce qui était caché.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Mais la Sagesse, où la trouver? Où est le siège de la Raison?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Le mortel n’en connaît pas le prix, elle est introuvable au pays des vivants.
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
L’Abîme dit: "Elle n’est pas dans mon sein!" Et la mer dit: "Elle n’est pas chez moi!"
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
On ne peut l’acquérir pour de l’or de choix, on ne l’achète pas au poids de l’argent.
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
L’Or d’Ophir ne correspond pas à sa valeur, ni l’onyx précieux, ni le saphir.
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Ni or ni verre ne peuvent rivaliser avec elle; aucun vase d’or fin ne paie son prix.
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
Ni corail ni cristal n’entrent en compte; la possession de la sagesse vaut mieux que les perles.
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
La topaze d’Ethiopie ne l’égale point; on ne peut la mettre en balance avec l’or pur.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Oui, la Sagesse d’où vient-elle? Où est le siège de la Raison?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Elle se dérobe aux yeux de tout vivant, elle est inconnue à l’oiseau du ciel.
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
L’Abîme et la mort disent: "De nos oreilles nous avons entendu parler d’elle."
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
C’Est Dieu qui en sait le chemin, c’est lui qui en connaît le siège.
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
Car ses regards portent jusqu’aux confins de la terre; tout ce qui est sous les cieux, il le voit.
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
Lorsqu’il donna au vent son équilibre et détermina la mesure des eaux,
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
lorsqu’il traça sa loi à la pluie et sa voie à l’éclair sonore,
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
c’est alors qu’il l’a vue et appréciée à sa valeur, c’est alors qu’il en a marqué la place et pénétré le fond,
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
et il a dit à l’homme: "Ah! La crainte du Seigneur, voilà la Sagesse; éviter le mal, voilà la Raison."

< Ayubu 28 >