< Ayubu 28 >

1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
Though there is, for silver, a vein, and a place for the gold they refine;
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Iron, out of the ore, is taken, and, stone, poureth out copper;
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
An end, hath one set to the darkness, and, into every extremity, is, he, making search, for the stone of darkness and death-shade;
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
He hath sunken a shaft, away from the inhabitants; Places forsaken by the foot, they hang down, away from men, sway to and fro;
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
As for the earth, out of it, cometh forth bread, and, under it, is upturned, as it were fire;
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
The place of sapphires, are the stones thereof, and it hath, nuggets of gold: —
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
A path, the vulture hath not discerned, nor hath the eye of the hawk scanned it;
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
Ravenous beasts have not made a track thereof, neither hath the lion marched thereon:
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
Upon the flint, hath he thrust forth his hand, He hath turned up mountains by the roots;
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
Among the rocks, hath he cut open streams, and, every precious thing, hath his eye seen:
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
From trickling, he restraineth, rivers, and, some hidden thing, is he bringing out to light.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Yet where can, Wisdom, be found? And where is the place of understanding?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Mortal knoweth not the way thereof, neither can it be found in the land of the living;
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
The resounding deep, hath said, It is not in me! And, the sea, hath said, It is not with me!
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
Pure gold cannot be given in its stead, neither can silver he weighed as the value thereof;
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
It cannot be put into the scales against the gold of Ophir, with costly onyx, or sapphire;
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Neither gold nor crystal can compare with it, nor can, the exchange thereof, be a vessel of pure gold,
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
Coral or crystal, cannot be mentioned, Yea, a possession, is wisdom, above red coral;
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
The topaz of Ethiopia cannot compare with it, Against purest gold, can it not be weighed.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Whence then cometh, wisdom? And where is the place of understanding?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Seeing it hath been hid from the eyes of every living thing, and, from the bird of the heavens, hath it been concealed?
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
Destruction and death, have said, With our ears, have we heard the report thereof!
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
GOD, understandeth the way thereof, and, he, discerneth the place thereof;
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
For, he, unto the ends of the earth, directeth his look, under all the heavens, he seeth;
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
Making, for the wind, a weight, and, the waters, he proved by measure,
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
When he made, for the rain, a decree, and a way for the lightning of thunders,
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
Then, saw he it, and declared it, He settled it, yea also he searched it out;
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
And said to the son of earth, Lo! the reverence of the Lord, that, is wisdom, and, to avoid evil, is understanding.

< Ayubu 28 >