< Ayubu 28 >

1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
Truly there is a vein for silver, And a place for gold, which men refine.
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Iron is obtained from earth, And stone is melted into copper.
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
Man putteth an end to darkness; He searcheth to the lowest depths For the stone of darkness and the shadow of death.
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
From the place where they dwell they open a shaft; Forgotten by the feet, They hang down, they swing away from men.
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
The earth, out of which cometh bread, Is torn up underneath, as it were by fire.
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
Her stones are the place of sapphires, And she hath clods of gold for man.
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
The path thereto no bird knoweth, And the vulture's eye hath not seen it;
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
The fierce wild beast hath not trodden it; The lion hath not passed over it.
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
Man layeth his hand upon the rock; He upturneth mountains from their roots;
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
He cleaveth out streams in the rocks, And his eye seeth every precious thing;
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
He bindeth up the streams, that they trickle not, And bringeth hidden things to light.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
But where shall wisdom be found? And where is the place of understanding?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Man knoweth not the price thereof, Nor can it be found in the land of the living.
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
The deep saith, It is not in me; And the sea saith, It is not with me.
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
It cannot be gotten for gold, Nor shall silver be weighed out as the price thereof.
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
It cannot be bought with the gold of Ophir, With the precious onyx or the sapphire.
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Gold and crystal are not to be compared with it; Nor can it be purchased with jewels of fine gold.
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
No mention shall be made of coral or of crystal; For wisdom is more precious than pearls.
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
The topaz of Ethiopia cannot equal it, Nor can it be purchased with pure gold.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Whence then cometh wisdom? And where is the place of understanding?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Since it is hidden from the eyes of all living, And kept close from the fowls of the air.
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
Destruction and Death say, We have heard a rumor of it with our ears.
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
God knoweth the way to it; He knoweth its dwelling-place.
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
For he seeth to the ends of the earth, And surveyeth all things under the whole heaven.
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
When he gave the winds their weight, And meted out the waters by measure;
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
When he prescribed a law to the rain, And a path to the thunder-flash, —
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
Then did he see it, and make it known; He established it, and searched it out.
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
But he said unto man, Behold, the fear of the Lord, that is wisdom, And to depart from evil is understanding.

< Ayubu 28 >