< Ayubu 28 >
1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
For there is a mine for silver, and a place for gold which they refine.
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Iron is taken out of the dust, and brass is molten out of the stone.
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
Man setteth an end to darkness, and searcheth out to the furthest bound the stones of thick darkness and of the shadow of death.
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
He breaketh open a shaft away from where men sojourn; they are forgotten of the foot that passeth by; they hang afar from men, they swing to and fro.
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
As for the earth, out of it cometh bread, and underneath it is turned up as it were by fire.
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
The stones thereof are the place of sapphires, and it hath dust of gold.
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
That path no bird of prey knoweth, neither hath the falcon's eye seen it;
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
The proud beasts have not trodden it, nor hath the lion passed thereby.
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
He putteth forth his hand upon the flinty rock; He overturneth the mountains by the roots.
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
He cutteth out channels among the rocks; and his eye seeth every precious thing.
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
He bindeth the streams that they trickle not; and the thing that is hid bringeth he forth to light.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
But wisdom, where shall it be found? And where is the place of understanding?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Man knoweth not the price thereof; neither is it found in the land of the living.
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
The deep saith: 'It is not in me'; and the sea saith: 'It is not with me.'
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
It cannot be gotten for gold, neither shall silver be weighed for the price thereof.
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
It cannot be valued with the gold of Ophir, with the precious onyx, or the sapphire.
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Gold and glass cannot equal it; neither shall the exchange thereof be vessels of fine gold.
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
No mention shall be made of coral or of crystal; yea, the price of wisdom is above rubies.
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
The topaz of Ethiopia shall not equal it, neither shall it be valued with pure gold.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Whence then cometh wisdom? And where is the place of understanding?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Seeing it is hid from the eyes of all living, and kept close from the fowls of the air.
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
Destruction and Death say: 'We have heard a rumor thereof with our ears.'
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
God understandeth the way thereof, and He knoweth the place thereof.
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
For He looketh to the ends of the earth, and seeth under the whole heaven;
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
When He maketh a weight for the wind, and meteth out the waters by measure.
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
When He made a decree for the rain, and a way for the storm of thunders;
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
Then did He see it, and declare it; He established it, yea, and searched it out.
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
And unto man He said: 'Behold, the fear of the Lord, that is wisdom; and to depart from evil is understanding.'