< Ayubu 23 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Ndipo Ayubu akajibu:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

< Ayubu 23 >