< Ayubu 23 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
ヨブこたへて曰く
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
我は今日にても尚つぶやきて服せず わが禍災はわが嘆息よりも重し
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
ねがはくは神をたづねて何處にか遇まつるを知り其御座に參いたらんことを
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
我この愁訴をその御前に陳べ口を極めて辨論はん
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
我その我に答へたまふ言を知り また其われに言たまふ所を了らん
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
かれ大なる能をもて我と爭ひたまはんや 然らじ反つて我を眷みたまふべし
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
彼處にては正義人かれと辨爭ふことを得 斯せば我を鞫く者の手を永く免かるべし
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
しかるに我東に往くも彼いまさず 西に往くも亦見たてまつらず
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
北に工作きたまへども遇まつらず 南に隱れ居たまへば望むべからず
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
わが平生の道は彼知たまふ 彼われを試みたまはば我は金のごとくして出きたらん
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
わが足は彼の歩履に堅く隨がへり 我はかれの道を守りて離れざりき
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
我はかれの唇の命令に違はず 我が法よりも彼の口の言語を重ぜり
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
かれは一に居る者にまします 誰か能かれをして意を變しめん 彼はその心に慾する所をかならず爲たまふ
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
然ば我に向ひて定めし事を必らず成就たまはん 是のごとき事を多く彼は爲たまふなり
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
是故に我かれの前に慄ふ 我考ふれば彼を懼る
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
神わが心を弱くならしめ 全能者われをして懼れしめたまふ
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
かく我は暗の來らぬ先わが面を黑暗の覆ふ前に打絶れざりき