< Ayubu 23 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Hiob antwortete und sprach:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Auch heute empört sich meine Klage; seine Hand drückt schwer auf mein Seufzen.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
O daß ich ihn zu finden wüßte, gelangen könnte bis zu seinem Richterstuhl!
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
So wollte ich vor ihm meine Sache darlegen und meinen Mund mit Beweisen füllen.
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
Ich möchte wissen, was er mir erwidern würde, und erfahren, was er zu mir sagen würde!
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Würde er in der Fülle der Macht mit mir streiten? Nein, nur achten würde er auf mich!
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
Dann würde ein Redlicher mit ihm rechten, und für immer machte ich mich von meinem Richter frei!
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
Doch - gehe ich ostwärts, so ist er nicht da, und westwärts - so gewahre ich ihn nicht.
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
Im Norden schafft er, aber ich sehe ihn nicht, biegt ab gen Süden - aber ich erblicke ihn nicht.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
Denn er weiß, welchen Wandel ich geführt - prüfte er mich, wie Gold würde ich hervorgehn.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
An seiner Spur hat fest mein Fuß gehalten, seinen Weg hab' ich verfolgt, ohne abzuweichen.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
Von seiner Lippen Vorschrift wich ich nie, barg in meiner Brust die Worte seines Munds.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
Er aber bleibt sich gleich - wer will ihm wehren? Sein Wille begehrt's, da führt er's aus!
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
Ja, er wird zu Ende führen, was er mir bestimmt hat, und solcherlei hat er noch vieles im Sinn.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
Darum erschrecke ich vor seinem Angesicht; überdenke ich's, so erbebe ich vor ihm.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
Ja, Gott hat meinen Mut gebrochen und der Allmächtige hat mich mit Schrecken erfüllt.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
Denn nicht des Unglücks wegen fühle ich mich vernichtet, noch wegen meiner Person, die Dunkel bedeckt hat.

< Ayubu 23 >