< Ayubu 23 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Job prit la parole et dit:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Maintenant encore ma plainte est une révolte, Mais la souffrance étouffe mes soupirs.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Oh! Si je savais où le trouver, Si je pouvais arriver jusqu’à son trône,
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
Je plaiderais ma cause devant lui, Je remplirais ma bouche d’arguments,
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
Je connaîtrais ce qu’il peut avoir à répondre, Je verrais ce qu’il peut avoir à me dire.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Emploierait-il toute sa force à me combattre? Ne daignerait-il pas au moins m’écouter?
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
Ce serait un homme droit qui plaiderait avec lui, Et je serais pour toujours absous par mon juge.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
Mais, si je vais à l’orient, il n’y est pas; Si je vais à l’occident, je ne le trouve pas;
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
Est-il occupé au nord, je ne puis le voir; Se cache-t-il au midi, je ne puis le découvrir.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
Il sait néanmoins quelle voie j’ai suivie; Et, s’il m’éprouvait, je sortirais pur comme l’or.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
Mon pied s’est attaché à ses pas; J’ai gardé sa voie, et je ne m’en suis point détourné.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
Je n’ai pas abandonné les commandements de ses lèvres; J’ai fait plier ma volonté aux paroles de sa bouche.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
Mais sa résolution est arrêtée; qui s’y opposera? Ce que son âme désire, il l’exécute.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
Il accomplira donc ses desseins à mon égard, Et il en concevra bien d’autres encore.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
Voilà pourquoi sa présence m’épouvante; Quand j’y pense, j’ai peur de lui.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
Dieu a brisé mon courage, Le Tout-Puissant m’a rempli d’effroi.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
Car ce ne sont pas les ténèbres qui m’anéantissent, Ce n’est pas l’obscurité dont je suis couvert.