< Ayubu 23 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then responded Job, and said: —
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Even to-day, is my complaint rebellion? His hand, is heavier than my groaning.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Oh that I knew where I might find him! I would come even unto his dwelling-place;
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
I would set out, before him, a plea, and, my mouth, would I fill with arguments;
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
I would note the words wherewith he would respond to me, and would mark what he would say to me.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Would he, with fulness of might, contend with me? Nay, surely, he, would give heed to me!
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
There an upright man, might reason with him, so should I deliver myself completely from my judge.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
Behold! eastward, I go, but he is not there, and, westward, but I perceive him not;
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
On the north, where he worketh, but I get no vision, He hideth himself on the south that I cannot see him.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
But, he, knoweth the way that I choose, Having tried me, as gold, I shall come forth.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
Of his steps, my foot taketh hold, His way, have I kept, and not swerved;
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
The command of his lips, and would not go back, and, in my bosom, have I treasured the words of his lips.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
But, he, is one, and who can turn him? What his soul desired, he hath done.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
Surely he will accomplish what is decreed for me, and, many such things, hath he in store.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
For this cause, from his presence, am I driven in fear, I diligently consider and am kept back from him in dread:
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
Yea, GOD, hath made timid my heart, and, the Almighty, hath put me in terror.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
Because I was not cut off before the darkness, nor, before my face, did the gloom form a shroud.

< Ayubu 23 >