< Ayubu 23 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Bvt Iob answered and sayd,
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Though my talke be this day in bitternes, and my plague greater then my groning,
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Would God yet I knew how to finde him, I would enter vnto his place.
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
I would pleade the cause before him, and fill my mouth with arguments.
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
I would knowe the wordes, that he would answere me, and would vnderstand what he would say vnto me.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Would he plead against me with his great power? No, but he would put strength in me.
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
There the righteous might reason with him, so I shoulde be deliuered for euer from my Iudge.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
Behold, if I go to the East, he is not there: if to the West, yet I can not perceiue him:
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
If to the North where he worketh, yet I cannot see him: he wil hide himselfe in the South, and I cannot beholde him.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
But he knoweth my way, and trieth mee, and I shall come forth like the gold.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
My foote hath followed his steps: his way haue I kept, and haue not declined.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
Neyther haue I departed from the commandement of his lippes, and I haue esteemed the words of his mouth more then mine appointed foode.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
Yet he is in one minde, and who can turne him? yea, he doeth what his minde desireth.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
For he will performe that, which is decreed of me, and many such things are with him.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
Therefore I am troubled at his presence, and in considering it, I am afraid of him.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
For God hath softened mine heart, and the Almightie hath troubled me.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
For I am not cut off in darknesse, but he hath hid the darkenesse from my face.