< Ayubu 23 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered, and said:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Now also my words are in bitterness, and the hand of my scourge is more grievous than my mourning.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Who will grant me that I might know and find him, and come even to his throne?
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
I would set judgment before him, and would fill my mouth with complaints.
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
That I might know the words that he would answer me, and understand what he would say to me.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
I would not that he should contend with me with much strength, nor overwhelm me with the weight of his greatness.
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
Let him propose equity against me, and let my judgment come to victory.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
But if I go to the east, he appeareth not; if to the west, I shall not understand him.
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
If to the left hand, what shall I do? I shall not take hold on him: if I turn myself to the right hand, I shall not see him.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
But he knoweth my way, and has tried me as gold that passeth through the fire:
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
My foot hath followed his steps, I have kept his way, and have not declined from it.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
I have not departed from the commandments of his lips, and the words of his mouth I have hid in my bosom.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
For he is alone, and no man can turn away his thought: and whatsoever is soul hath desired, that hath he done.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
And when he shall have fulfilled his will in me, many other like things are also at hand with him.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
And therefore I am troubled at his presence, and when I consider him I am made pensive with fear.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
God hath softened my heart, and the Almighty hath troubled me.
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
For I have not perished because of the darkness that hangs over me, neither hath the mist covered my face.