< Ayubu 22 >

1 Kisha Elifazi Mtemani akajibu na kusema,
ויען אליפז התמני ויאמר׃
2 Je mtu anaweza kumfaa Mungu “Je mwenye hekima anaweza kufaa kwake.
הלאל יסכן גבר כי יסכן עלימו משכיל׃
3 Je inafurahisha kwa Mwenyezi ikiwa u mwenye haki? Je ni faida yake ukiyafanya safi maisha yako?
החפץ לשדי כי תצדק ואם בצע כי תתם דרכיך׃
4 Je ni kwa sababu ya uchaji wako kwake hata akukemee na kukuadhibu?
המיראתך יכיחך יבוא עמך במשפט׃
5 Je si kwa sababu ya wingi wa uovu wako? Je hakuna mwisho wa makosa yako?
הלא רעתך רבה ואין קץ לעונתיך׃
6 Kwa maana umechukua dhamana kutoka kwa ndugu yako bila sababu; umechukua mavazi ya mtu na kumwacha uchi.
כי תחבל אחיך חנם ובגדי ערומים תפשיט׃
7 Haukuwapa wenye kiu maji ya kunywea; umewanyima chakula wenye njaa
לא מים עיף תשקה ומרעב תמנע לחם׃
8 japokuwa wewe, mwenye uwezo, uliimiliki nchi, japokuwa wewe, mwenye kuheshimiwa, uliishi ndani yake.
ואיש זרוע לו הארץ ונשוא פנים ישב בה׃
9 Umewaacha wajane waondoke bila kitu; umewatesa yatima.
אלמנות שלחת ריקם וזרעות יתמים ידכא׃
10 Kwa hiyo, mabaya yanakuzunguka, na hofu za ghafla zinakusumbua.
על כן סביבותיך פחים ויבהלך פחד פתאם׃
11 Kuna giza, hata usione; gharika inakufunika.
או חשך לא תראה ושפעת מים תכסך׃
12 Je Mungu hayupo juu mbinguni? Anaangalia juu ya nyota, jinsi zilivyo juu!
הלא אלוה גבה שמים וראה ראש כוכבים כי רמו׃
13 Unasema, 'Mungu anajua nini? Je anaweza kuamua kupitia giza totoro?
ואמרת מה ידע אל הבעד ערפל ישפוט׃
14 Mawingu ni kifuniko chake, hata asituone; anatembea anga la mbinguni.'
עבים סתר לו ולא יראה וחוג שמים יתהלך׃
15 Je utayaishi maisha ya zamani walioishi waovu -
הארח עולם תשמר אשר דרכו מתי און׃
16 walioondolewa kabla ya siku zao, ambao misingi yao imeondolewa kama mto,
אשר קמטו ולא עת נהר יוצק יסודם׃
17 waliomwambia Mungu, 'Ondoka kwetu'; waliosema, 'Mwenyezi anaweza kututenda nini?
האמרים לאל סור ממנו ומה יפעל שדי למו׃
18 Hata hivyo bado alizijaza nyumba zao kwa mema; mipango ya waovu iko mbali nami.
והוא מלא בתיהם טוב ועצת רשעים רחקה מני׃
19 Wenye haki wanayaona yawapatayo waovu na kufurahi; wasio na hatia wanawacheka kwa dhihaka.
יראו צדיקים וישמחו ונקי ילעג למו׃
20 Wanasema, 'Bila shaka walioinuka kinyume chetu wameondolewa; moto umeteketeza mali zao.'
אם לא נכחד קימנו ויתרם אכלה אש׃
21 Basi patana na Mungu na uwe na amani naye; kwa njia hiyo, mema yatakujia.
הסכן נא עמו ושלם בהם תבואתך טובה׃
22 Nakusihi, pokea, maelekezo yake; uyatii maneno yake.
קח נא מפיו תורה ושים אמריו בלבבך׃
23 Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa, ukiacha kutenda uovu makaoni mwako.
אם תשוב עד שדי תבנה תרחיק עולה מאהלך׃
24 Weka hazina zako mavumbini, dhahabu ya Ofiri kati ya mawe ya vijito,
ושית על עפר בצר ובצור נחלים אופיר׃
25 na Mwenyezi atakuwa hazina zako, fedha ya thamani kwako.
והיה שדי בצריך וכסף תועפות לך׃
26 Nawe utajifurahisha katika Mwenyezi; utamwangalia Mungu.
כי אז על שדי תתענג ותשא אל אלוה פניך׃
27 Utamwomba, naye atakusikiliza; utamtolea nadhiri.
תעתיר אליו וישמעך ונדריך תשלם׃
28 Lakini pia utatamka lolote, nawe utapewa; nuru itaangaza maishani mwako.
ותגזר אומר ויקם לך ועל דרכיך נגה אור׃
29 Mungu humshusha mwenye kiburi, naye humwinua mnyenyekevu.
כי השפילו ותאמר גוה ושח עינים יושע׃
30 Atamwokoa asiye na hatia; utaokolewa kupitia usafi wa mikono yako.”
ימלט אי נקי ונמלט בבר כפיך׃

< Ayubu 22 >