< Ayubu 22 >

1 Kisha Elifazi Mtemani akajibu na kusema,
ויען אליפז התמני ויאמר
2 Je mtu anaweza kumfaa Mungu “Je mwenye hekima anaweza kufaa kwake.
הלאל יסכן-גבר-- כי-יסכן עלימו משכיל
3 Je inafurahisha kwa Mwenyezi ikiwa u mwenye haki? Je ni faida yake ukiyafanya safi maisha yako?
החפץ לשדי כי תצדק ואם-בצע כי-תתם דרכיך
4 Je ni kwa sababu ya uchaji wako kwake hata akukemee na kukuadhibu?
המיראתך יכיחך יבוא עמך במשפט
5 Je si kwa sababu ya wingi wa uovu wako? Je hakuna mwisho wa makosa yako?
הלא רעתך רבה ואין-קץ לעונתיך
6 Kwa maana umechukua dhamana kutoka kwa ndugu yako bila sababu; umechukua mavazi ya mtu na kumwacha uchi.
כי-תחבל אחיך חנם ובגדי ערומים תפשיט
7 Haukuwapa wenye kiu maji ya kunywea; umewanyima chakula wenye njaa
לא-מים עיף תשקה ומרעב תמנע-לחם
8 japokuwa wewe, mwenye uwezo, uliimiliki nchi, japokuwa wewe, mwenye kuheshimiwa, uliishi ndani yake.
ואיש זרוע לו הארץ ונשוא פנים ישב בה
9 Umewaacha wajane waondoke bila kitu; umewatesa yatima.
אלמנות שלחת ריקם וזרעות יתמים ידכא
10 Kwa hiyo, mabaya yanakuzunguka, na hofu za ghafla zinakusumbua.
על-כן סביבותיך פחים ויבהלך פחד פתאם
11 Kuna giza, hata usione; gharika inakufunika.
או-חשך לא-תראה ושפעת-מים תכסך
12 Je Mungu hayupo juu mbinguni? Anaangalia juu ya nyota, jinsi zilivyo juu!
הלא-אלוה גבה שמים וראה ראש כוכבים כי-רמו
13 Unasema, 'Mungu anajua nini? Je anaweza kuamua kupitia giza totoro?
ואמרת מה-ידע אל הבעד ערפל ישפוט
14 Mawingu ni kifuniko chake, hata asituone; anatembea anga la mbinguni.'
עבים סתר-לו ולא יראה וחוג שמים יתהלך
15 Je utayaishi maisha ya zamani walioishi waovu -
הארח עולם תשמור-- אשר דרכו מתי-און
16 walioondolewa kabla ya siku zao, ambao misingi yao imeondolewa kama mto,
אשר-קמטו ולא-עת נהר יוצק יסודם
17 waliomwambia Mungu, 'Ondoka kwetu'; waliosema, 'Mwenyezi anaweza kututenda nini?
האמרים לאל סור ממנו ומה-יפעל שדי למו
18 Hata hivyo bado alizijaza nyumba zao kwa mema; mipango ya waovu iko mbali nami.
והוא מלא בתיהם טוב ועצת רשעים רחקה מני
19 Wenye haki wanayaona yawapatayo waovu na kufurahi; wasio na hatia wanawacheka kwa dhihaka.
יראו צדיקים וישמחו ונקי ילעג-למו
20 Wanasema, 'Bila shaka walioinuka kinyume chetu wameondolewa; moto umeteketeza mali zao.'
אם-לא נכחד קימנו ויתרם אכלה אש
21 Basi patana na Mungu na uwe na amani naye; kwa njia hiyo, mema yatakujia.
הסכן-נא עמו ושלם בהם תבואתך טובה
22 Nakusihi, pokea, maelekezo yake; uyatii maneno yake.
קח-נא מפיו תורה ושים אמריו בלבבך
23 Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa, ukiacha kutenda uovu makaoni mwako.
אם-תשוב עד-שדי תבנה תרחיק עולה מאהלך
24 Weka hazina zako mavumbini, dhahabu ya Ofiri kati ya mawe ya vijito,
ושית-על-עפר בצר ובצור נחלים אופיר
25 na Mwenyezi atakuwa hazina zako, fedha ya thamani kwako.
והיה שדי בצריך וכסף תועפות לך
26 Nawe utajifurahisha katika Mwenyezi; utamwangalia Mungu.
כי-אז על-שדי תתענג ותשא אל-אלוה פניך
27 Utamwomba, naye atakusikiliza; utamtolea nadhiri.
תעתיר אליו וישמעך ונדריך תשלם
28 Lakini pia utatamka lolote, nawe utapewa; nuru itaangaza maishani mwako.
ותגזר-אמר ויקם לך ועל-דרכיך נגה אור
29 Mungu humshusha mwenye kiburi, naye humwinua mnyenyekevu.
כי-השפילו ותאמר גוה ושח עינים יושע
30 Atamwokoa asiye na hatia; utaokolewa kupitia usafi wa mikono yako.”
ימלט אי-נקי ונמלט בבר כפיך

< Ayubu 22 >