< Ayubu 21 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Toda Job je odgovoril in rekel:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
»Marljivo prisluhnite mojemu govoru in to naj bodo vaše tolažbe.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Pustite mi, da lahko govorim in potem, ko bom govoril, zasmehujte.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Kar se mene tiče ali je moja pritožba proti človeku? In če bi bilo tako, zakaj naj potem moj duh ne bi bil nemiren?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Poglejte me in bodite osupli in svojo roko položite na svoja usta.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Celo kadar se spomnim, sem prestrašen in trepetanje se oprijemlje mojega mesa.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Zakaj zlobni živijo, postanejo stari in so mogočni v moči?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Njihovo seme je z njimi utrjeno v njihovem pogledu in njihovo potomstvo pred njihovimi očmi.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Njihove hiše so varne pred strahom niti nad njimi ni Božje palice.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Njihov bik plodi in ne odpove; njihova krava povrže in ne zavrže svojega teleta.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Svoje malčke pošiljajo kakor trop in njihovi otroci plešejo.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Vzamejo tamburin in harfo in se veselijo ob zvoku piščali.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
Svoje dni preživijo v obilju in v trenutku gredo dol v grob. (Sheol h7585)
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Zato Bogu rečejo: ›Odidi od nas, kajti mi ne želimo spoznanja tvojih poti.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Kaj je Vsemogočni, da bi mu služili? In kakšno korist bi imeli, če molimo k njemu?‹
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Glej, njihovo dobro ni v njihovi roki; nasvet zlobnega je daleč od mene.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
Kako pogosto je sveča zlobnih ugasnjena! In kako pogosto nanje prihaja njihovo uničenje! Bog v svoji jezi deli bridkosti.
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
So kakor strnišče pred vetrom in kakor pleve, ki jih vihar odnaša proč.
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Bog kopiči njegovo krivičnost za njegove otroke. Nagrajuje ga in on bo to vedel.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Njegove oči bodo videle njegovo uničenje in pil bo od besa Vsemogočnega.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Kajti kakšen užitek ima on v njegovi hiši za njim, ko je število njegovih mesecev na sredi prekinjeno?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Mar bo kdorkoli Boga učil spoznanja? Ker on sodi tiste, ki so visoko.
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Nekdo umre v svoji polni moči, v celoti spokojen in tiho.
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
Njegove prsi so polne mleka in njegove kosti so navlažene z mozgom.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Drugi pa umira v grenkobi svoje duše in nikoli ne jé z užitkom.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Podobno se bodo ulegli v prah in ličinke jih bodo pokrile.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Glej, poznam vaše misli in naklepe, ki ste jih krivično domišljali zoper mene.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Kajti pravite: »Kje je prinčeva hiša? Kje so bivališča zlobnih?
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Mar jih niste prosili, da gredo po poti? Ali poznate njihove simbole,
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
da je zlobni prihranjen za dan uničenja? Privedeni bodo k dnevu besa.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
Kdo bo njegovo pot oznanil njegovemu obrazu? Kdo mu bo poplačal, kar je storil?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Vendar bo priveden h grobu in ostal bo v gomili.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Grude iz doline mu bodo sladke in vsak človek bo priveden za njim, kakor so tam brezštevilni pred njim.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Kako me potem zaman tolažite, glede na to, da v vaših odgovorih ostaja neresnica?«

< Ayubu 21 >