< Ayubu 21 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Då svara Job og sagde:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
«Å høyr då, høyr på mine ord! Gjev i minsto det til trøyst!
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Lat meg få lov å tala ut, so kann du spotta etterpå.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Klagar eg vel på menneskje? Og hev eg ikkje grunn til harm?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Vend dykk til meg, og ottast so; legg handi so på dykkar munn.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Eg støkk, når eg det kjem i hug; ei bivring gjenom kroppen gjeng.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Kvifor fær dei gudlause liva, auka i magt som åri gjeng?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Dei ser si ætt stå fast ikring deim, dei hev sitt avkjøme for augo.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
I fred stend husi deira trygge, Guds svipa råkar ikkje deim;
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
med heppa parast deira fe, og kyrne kastar aldri kalv.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Dei slepper borni ut som lamb, og gutarne i leiken hoppar;
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Dei syng til trumma og til cither og frygdar seg ved fløyteljod.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
I lukka liver dei si tid og fer so brått til helheim ned. (Sheol h7585)
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Til Gud dei segjer: «Haldt deg burte!» Me vil’kje kjenna dine vegar!
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Kvi skal me tena den Allsterke? Kva gagnar det å be til honom?»
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
«Dei hev’kje lukka si i handi» - Langt burt frå meg med gudlaus råd!
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
Når sloknar lampa for gudlause? Når kjem ulukka yver deim? Gjev han deim straff i vreidesmod?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
Fer dei vel burt som strå for vind, lik agner som i stormen fyk?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
«Gud gøymer straffi til hans born.» Nei, sjølv skal mannen straffi kjenna!
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Lat han få sjå sitt eige fall og drikka harm frå den Allsterke!
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Kva bryr han seg vel um sitt hus, når månadstalet hans er fullt?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Vil nokon hjelpa Gud til kunnskap, han som er domar for dei høgste?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Den eine døyr på velmagts høgd, fullkomleg trygg og fredeleg;
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
hans fat er fulle utav mjølk, og i hans bein er mergen frisk;
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
den andre døyr so beisk i hug, hev ingenting av lukka smaka.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Dei båe vert i moldi lagde, og deira klednad makkar er.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Sjå kor eg kjennar dykkar tankar, og dykkar meinkrokar mot meg.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
De spør: «Kvar er vel stormannshuset? Kvar er det tjeld der gudlause bur?»
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Hev de’kje høyrt av ferdafolk - de trur vel det som dei fortel -:
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
«Den vonde frå ulukka slepp; han berga vert på vreidedagen.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
Kven lastar honom for hans ferd? Og straffar honom for hans gjerd?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Han vert til gravi båren burt, og ved hans gravhaug held dei vakt.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Søtt søv han under torv i dal, og i hans far all verdi fer, som tallause gjekk fyre honom.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Det trøystar meg med tome ord; av dykkar svar er sviket att.»

< Ayubu 21 >