< Ayubu 21 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Mais Job répondit, et dit:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
Ecoutez attentivement mon discours, et cela me tiendra lieu de consolations de votre part.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Supportez-moi, et je parlerai, et après que j'aurai parlé, moquez-vous.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Pour moi, mon discours s'adresse-t-il à un homme? si cela était, comment mon esprit ne défaudrait-il pas?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Regardez-moi, et soyez étonnés, et mettez la main sur la bouche.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Quand je pense à [mon état], j'en suis tout étonné, et un tremblement saisit ma chair.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Pourquoi les méchants vivent-ils, [et] vieillissent, et même pourquoi sont-ils les plus puissants?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Leur race se maintient en leur présence avec eux, et leurs rejetons s'élèvent devant leurs yeux.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Leurs maisons jouissent de la paix loin de la frayeur; la verge de Dieu n'est point sur eux.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Leur vache conçoit, et n'y manque point; leur jeune vache se décharge de son veau, et n'avorte point.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Ils font sortir devant eux leurs petits, comme un troupeau de brebis, et leurs enfants sautent.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Ils sautent au son du tambour et du violon, et se réjouissent au son des orgues.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
Ils passent leurs jours dans les plaisirs, et en un moment ils descendent au sépulcre. (Sheol )
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Cependant ils ont dit au [Dieu] Fort: Retire-toi de nous; car nous ne nous soucions point de la science de tes voies.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Qui est le Tout-puissant que nous le servions? et quel bien nous reviendra-t-il de l'avoir invoqué?
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Voilà, leur bien n'est pas en leur puissance. Que le conseil des méchants soit loin de moi!
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
Aussi combien de fois arrive-t-il que la lampe des méchants est éteinte, et que l'orage vient sur eux! [Dieu] leur distribuera leurs portions en sa colère.
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
Ils seront comme la paille exposée au vent, et comme la balle qui est enlevée par le tourbillon.
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Dieu réservera aux enfants du méchant la punition de ses violences, il la leur rendra, et il le saura.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Ses yeux verront sa ruine, et il boira [le calice de] la colère du Tout-puissant.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Et quel plaisir aura-t-il en sa maison, laquelle il laisse après soi, puisque le nombre de ses mois aura été retranché?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Enseignerait-on la science au [Dieu] Fort, à lui qui juge ceux qui sont élevés?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
L'un meurt dans toute sa vigueur, tranquille et en repos;
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
Ses vaisseaux sont remplis de lait, et ses os sont abreuvés de moëlle.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Et l'autre meurt dans l'amertume de son âme, et n'ayant jamais fait bonne chère.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Et néanmoins ils sont couchés également dans la poudre, et les vers les couvrent.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Voilà, je connais vos pensées, et les jugements que vous formez contre moi.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Car vous dites: Où est la maison de cet homme si puissant, et où est la tente dans laquelle les méchants demeuraient?
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Ne vous êtes-vous jamais informés des voyageurs, et n'avez-vous pas appris par les rapports qu'ils vous ont faits,
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
Que le méchant est réservé pour le jour de la ruine, pour le jour que les fureurs sont envoyées?
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
[Mais] qui le reprendra en face de sa conduite? et qui lui rendra le mal qu'il a fait?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Il sera néanmoins porté au sépulcre, et il demeurera dans le tombeau.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Les mottes des vallées lui sont agréables; et tout le monde s'en va à la file après lui, et des gens sans nombre marchent au-devant de lui.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Comment donc me donnez-vous des consolations vaines, puisqu'il y a toujours de la prévarication dans vos réponses?