< Ayubu 21 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Or Job reprenant dit:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
Ecoutez, écoutez mes raisonnements, afin que de telles consolations me soient épargnées.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Dussiez-vous me maudire je parlerai, ensuite vous ne rirez plus de moi.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Qu'y a-t-il? Mes reproches s'adressent-il à un homme? Et pourquoi donc contiendrais-je ma colère?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Lorsque vous m'aurez examiné à fond vous serez saisis de surprise, et de vous mains vous vous frapperez les joues.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Car si je recueille mes souvenirs, je n'ai eu que zèle pur, et les douleurs affligent mes chairs.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Pourquoi les impies vivent-ils, et vieillissent-ils au sein de la richesse?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Leur famille est selon leur âme, ils ont leurs enfants sous les yeux.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Leurs maisons prospèrent, on n'y ressent aucune crainte, car le fouet du Seigneur n'est point dirigé contre eux.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Pas d'avortement parmi leurs génisses, leurs bêtes pleines portent sans mal; et, à terme, elles mettent bas leurs fruits.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Leurs menus troupeaux ne diminuent jamais, et leurs enfants dansent
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Au son de la harpe et de la cithare, et ils se complaisent au chant des cantiques.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
Leur vie s'est écoulée au milieu des biens, et ils se sont endormis dans le repos du sépulcre. (Sheol )
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Cependant ils ont dit au Seigneur: Détournez-vous de nous; nous n'avons que faire de connaître vos voies.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Qu'est-ce donc que le Tout-Puissant pour que nous le servions? Qu'est-il besoin que nous allions au devant de lui?
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Leurs mains sont pleines de richesses, et le Seigneur ne surveille pas les œuvres des impies.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
Il est vrai qu'il advient aussi que leur lampe s'éteigne; ils essuient des catastrophes; des douleurs leur sont envoyées par la colère de Dieu.
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
Ils seront alors comme de la paille que le vent emporte, ou comme le tourbillon de poussière qu'une tempête fait voler.
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Que les richesses du méchant échappent à ses fils; le Seigneur le rétribuera et il saura pourquoi.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Que ses yeux voient sa propre immolation; qu'il ne soit pas épargné par le Seigneur.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Car la volonté de Dieu est avec lui dans sa maison, et son nombre de mois lui a été compté.
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Le Seigneur n'et-il pas le seul qui distribue l'intelligence et le savoir? Seul il juge les scélérats.
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Tel mourra dans la plénitude de son innocence, complètement heureux et bien portant;
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
Les entrailles pleines de graisse et regorgeant de mœlle.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Un autre finit en l'amertume de son âme, sans avoir jamais rien mangé de bon.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Ils dorment ensemble sous la terre; la pourriture les enveloppe.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Je sais votre hardiesse à m'accuser.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Ainsi vous demanderez: Où donc est la maison du chef? qu'est devenue la tente qui abritait des criminels?
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Interrogez les voyageurs et ne faussez pas leurs témoignages.
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
Ils vous diront que le fardeau du méchant est allégé le jour de sa perte; on l'en déchargera tout à fait le jour de la colère du Seigneur.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
Qui donc lui montrera en face ses voies et ce qu'il a fait? Qui se chargera de le punir?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
On le portera au lieu des sépultures, et il a veillé lui-même à la construction de sa tombe.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Sa présence réjouit jusqu'aux cailloux du torrent; chacun se fait un devoir de le suivre, et il est précédé d'une foule innombrable.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Comment donc me consolez-vous en vain? Car vous n'avez nullement adouci mes maux.