< Ayubu 21 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Job reprit la parole et dit:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
Daignez écouter mes paroles: je ne vous demande pas d’autres consolations.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Faites-moi un peu crédit pour que je puisse parler, et quand j’aurai fini, libre à vous de me railler.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Est-ce donc contre des hommes que mes plaintes sont dirigées? Dès lors pourquoi ma patience ne serait-elle pas à bout?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Tournez-vous vers moi et soyez stupéfaits, et posez la main sur la bouche.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Moi-même, en évoquant mes souvenirs, je suis consterné, et un frisson d’horreur s’empare de mon corps.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Pourquoi les méchants demeurent-ils en vie? Pourquoi vont-ils progressant et croissant en puissance?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Leur postérité est fortement établie devant eux, avec eux: leurs descendants sont là sous leurs yeux.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Leurs maisons sont en paix, à l’abri de toute crainte; la verge de Dieu ne les atteint pas.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Leurs taureaux s’accouplent et ne sont pas stériles; leurs génisses mettent bas et ne perdent pas leurs petits.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Ils envoient dehors leurs jeunes garçons comme un troupeau de brebis, et leurs enfants se livrent à leurs ébats.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Ils entonnent des chants en s’accompagnant du tambourin et du luth, et ils s’égaient aux sons de la flûte.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
Ils consument leurs jours dans le bonheur et, en un instant, ils descendent au Cheol. (Sheol )
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Et pourtant ils disent à Dieu: "Laisse-nous, nous n’avons nulle envie de connaître tes voies.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Qu’est-ce que le Tout-Puissant, que nous le servions? Quel profit aurons-nous à lui adresser des prières?"
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Assurément, ce n’est pas à leurs mains qu’ils sont redevables de leur bien-être. (Puisse toutefois le conseil des méchants être loin de moi!)
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
Arrive-t-il souvent que la lampe des impies s’éteigne, que le malheur fonde sur eux et que Dieu leur assigne dans sa colère le sort qu’ils méritent?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
Arrive-t-il souvent qu’ils soient comme la paille emportée par le vent, comme le chaume qu’enlève la tempête?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Dieu dira-t-on réserve à ses enfants le châtiment de ses crimes: mais qu’il l’inflige donc à lui-même, pour qu’il s’en ressente!
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Que ses propres yeux soient témoins de sa chute et qu’il s’abreuve de la colère de Dieu!
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Car quel intérêt peut-il porter à sa maison, quand il ne sera plus, puisque le nombre de ses années est fixé d’avance?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Est-ce à Dieu qu’on enseignera ce qui est raisonnable, à lui qui juge avec une autorité souveraine?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Celui-ci meurt au fort de sa vigueur, en pleine quiétude, en pleine paix,
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
alors que ses récipients débordent de lait, et que la moelle de ses os est abondamment pourvue.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Celui-là meurt, l’âme rassasiée d’amertume, sans avoir goûté le bonheur.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Et tous deux sont couchés dans la poussière et deviennent également la proie de la pourriture.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Eh quoi! Je connais vos intentions et les arrière-pensées que vous nourrissez injustement contre moi,
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
quand vous dites: "Où est la maison de l’homme important? Où, la tente habitée par les méchants?"
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Eh bien! Interrogez ceux qui parcourent le monde et ne méconnaissez pas les preuves qu’ils apportent:
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
c’est qu’au jour du désastre le méchant est épargné; au jour des violentes colères, il est tiré du danger.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
Qui lui jettera sa conduite à la face? Et ce qu’il a fait, qui le lui paiera?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
On le porte en pompe au lieu de sépulture, et on veille sur son mausolée.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Légères lui sont les glèbes de la vallée; tout le monde se traîne à sa suite; comme il a été précédé d’une innombrable multitude.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Comment donc m’offrirez-vous de vaines consolations? De toutes vos répliques il ne demeure qu’une criarde injustice.