< Ayubu 21 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Alors Job répondit,
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
« Écoutez attentivement mon discours. Que ceci soit votre consolation.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Permettez-moi, et je parlerai aussi. Après que j'ai parlé, moquez-vous.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
Quant à moi, ma plainte est-elle adressée à un homme? Pourquoi ne devrais-je pas être impatient?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Regardez-moi, et soyez étonnés. Posez votre main sur votre bouche.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Quand je me souviens, je suis troublé. L'horreur s'empare de ma chair.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
« Pourquoi les méchants vivent-ils, devenir vieux, oui, et devenir puissant?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Leur enfant est établi avec eux à leurs yeux, leur progéniture devant leurs yeux.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Leurs maisons sont à l'abri de la peur, la verge de Dieu n'est pas non plus sur eux.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Leurs taureaux se reproduisent sans faute. Leurs vaches vêlent, et ne font pas de fausses couches.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Ils envoient leurs petits comme un troupeau. Leurs enfants dansent.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Ils chantent au tambourin et à la harpe, et se réjouir au son de la pipe.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
Ils passent leurs jours dans la prospérité. En un instant, ils descendent au Shéol. (Sheol )
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Ils disent à Dieu: « Éloigne-toi de nous! car nous ne voulons pas connaître vos habitudes.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
Qu'est-ce que le Tout-Puissant, pour que nous le servions? Quel profit devrions-nous avoir, si nous le prions? ».
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Voici, leur prospérité n'est pas dans leur main. Le conseil des méchants est loin de moi.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
« Combien de fois la lampe des méchants s'éteint-elle? que leur calamité s'abat sur eux, que Dieu distribue des peines dans sa colère?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
Combien de fois ne sont-ils pas comme du chaume devant le vent? comme de l'ivraie que la tempête emporte?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Vous dites: « Dieu fait retomber son iniquité sur ses enfants ». Qu'il s'en rende compte à lui-même, afin qu'il le sache.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Que ses propres yeux voient sa destruction. Qu'il boive la colère du Tout-Puissant.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Car que se soucie-t-il de sa maison après lui, lorsque le nombre de ses mois sera interrompu?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
« Si quelqu'un enseigne la connaissance à Dieu, puisqu'il juge ceux qui sont élevés?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
On meurt dans toute sa force, en étant tout à fait à l'aise et tranquille.
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
Ses seaux sont pleins de lait. La mœlle de ses os est humidifiée.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Un autre meurt dans l'amertume de l'âme, et n'a jamais le goût du bien.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Ils se couchent tous deux dans la poussière. Le ver les recouvre.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
« Voici, je connais tes pensées, les plans avec lesquels vous me feriez du tort.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Car vous dites: « Où est la maison du prince? Où est la tente dans laquelle vivaient les méchants?
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
N'avez-vous pas demandé aux hommes de bonne volonté? Vous ne connaissez pas leurs preuves,
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
que l'homme mauvais est réservé pour le jour de la calamité, qu'ils sont conduits au jour de la colère?
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
Qui déclarera sa voie à sa face? Qui lui rendra ce qu'il a fait?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Pourtant, il sera porté au tombeau. Des hommes veilleront sur la tombe.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Les mottes de la vallée lui seront douces. Tous les hommes le suivront, comme il y en a eu d'innombrables avant lui.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
Alorscomment pouvez-vous me réconforter avec des bêtises, parce que dans vos réponses il ne reste que le mensonge? »