< Ayubu 20 >
1 Ndipo Sofari, Mnaamathi alijibu na kusema,
And Zophar the Naamathite answered and said,
2 “Mawazo yangu yananifanya mimi nijibu kwa haraka kwa sababu ya mashaka yaliyomo ndani yangu mimi.
Therefore do my thoughts give me an answer, and for this is my haste within me.
3 Mimi ninasikia kukemewa ambako kunaniondolea heshima mimi, lakini roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.
I hear a reproof putting me to shame; and [my] spirit answereth me by mine understanding.
4 Je, unafahamu kwamba ukweli huu kutoka enzi za kale, wakati Mungu alipomweka mwanadamu juu ya nchi:
Knowest thou [not] this, that of old, since man was placed upon earth,
5 ushindi wa mtu mwovu ni mfupi, na furaha ya mtu asiyemcha Mungu hudumu kwa kitambo tu?
The exultation of the wicked is short, and the joy of the ungodly man but for a moment?
6 Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu, na kichwa chake yeye kufikia kwenye mawingu,
Though his height mount up to the heavens, and his head reach unto the clouds,
7 bado mtu huyo atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe; wale waliokuwa wamemuona yeye watasema, 'Yuko wapi yeye'?
Like his own dung doth he perish for ever; they which have seen him shall say, Where is he?
8 Yeye atapaa mbali kama ndoto na hataonekana; ndivyo ilivyo, yeye atakuwa amefukuzwa mbali kama ono la
He flieth away as a dream, and is not found; and is chased away as a vision of the night.
9 usiku. Jicho ambalo lilimuona yeye halitamuona yeye tena; mahali pake hapatamuona yeye tena.
The eye which saw him shall [see him] not again; and his place beholdeth him no more.
10 Watoto wake wataomba msamaha kwa watu maskini, mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.
His children shall seek the favour of the poor, and his hands restore his wealth.
11 Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani, lakini zitalala naye chini katika mavumbi.
His bones were full of his youthful strength; but it shall lie down with him in the dust.
12 Japokuwa uovu ni mtamu katika mdomo wake yeye, japokuwa yeye anauficha chini ya ulimi wake yeye,
Though wickedness be sweet in his mouth [and] he hide it under his tongue,
13 japokuwa anaushikilia pale na hauruhusu kwenda lakini bado huushikilia katika mdomo wake yeye -
[Though] he spare it, and forsake it not, but keep it within his mouth,
14 chakula katika koromeo lake yeye hugeuka kuwa uchungu; hugeuka kuwa sumu ya majoka ndani yake yeye.
His food is turned in his bowels; it is the gall of asps within him.
15 Yeye humeza chini utajiri, lakini yeye atautapika tena; Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake yeye.
He hath swallowed down riches, but he shall vomit them up again: God shall cast them out of his belly.
16 Yeye atamumunya sumu ya majoka; ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.
He shall suck the poison of asps; the viper's tongue shall kill him.
17 Yeye hatafurahia vijito vya maji, wingi wa asali na siagi.
He shall not see streams, rivers, brooks of honey and butter.
18 Yeye atayarudisha matunda ya kazi yake na hataweza kuyala; yeye hatafurahia utajiri alioupata kwa biashara zake yeye.
That which he laboured for shall he restore, and not swallow down; its restitution shall be according to the value, and he shall not rejoice [therein].
19 Kwa kuwa yeye amewakandamiza na kuwasahau watu maskini; yeye kwa uonevu, amezichukua mbali nyumba ambazo hakuzijenga yeye.
For he hath oppressed, hath forsaken the poor; he hath violently taken away a house that he did not build.
20 Kwa sababu yeye mwenyewe hakujua utoshelevu wowote, yeye hataweza kuokoa kitu chochote katika kile ambacho alijifurahisha.
Because he knew no rest in his craving, he shall save nought of what he most desired.
21 Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza; kwa hiyo mafanikio yake yeye hayatakuwa ya kudumu.
Nothing escaped his greediness; therefore his prosperity shall not endure.
22 katika wingi wa utajiri wake yeye ataanguka katika mahangaiko; mkono wa kila mmoja ambaye yuko katika umaskini utakuja kinyume chake yeye.
In the fulness of his sufficiency he shall be in straits; every hand of the wretched shall come upon him.
23 Wakati akiwa katika kulijaza tumbo lake, Mungu atatupa hasira ya ghadhabu yake juu yake yeye; Mungu ataunyeshea chini juu yake yeye wakati yeye anakula.
It shall be that, to fill his belly, he will cast his fierce anger upon him, and will rain it upon him into his flesh.
24 Ingawa mtu huyo atakimbia kutoka katika silaha ya chuma, upinde wa shaba utampiga yeye.
If he have fled from the iron weapon, the bow of brass shall strike him through.
25 Mshale utatoboa kupitia mgongoni mwake na utatokezea; ni dhahiri, ncha inayong'ra itatokezea nje kupitia ini lake yeye; watesi huja tena juu yake.
He draweth it forth; it cometh out of his body, and the glittering point out of his gall: terrors are upon him.
26 Giza lliilo kamilika limetunzwa kwa akiba zake; moto usiopulizwa utamla yeye kwa haraka; utameza kile kilichoachwa katika hema yake.
All darkness is laid up for his treasures: a fire not blown shall devour him; it shall feed upon what is left in his tent.
27 Mbingu zitauweka wazi uovu wake, na nchi itainuka juu dhidi yake yeye kama shahidi.
The heavens shall reveal his iniquity, and the earth shall rise up against him.
28 Utajiri wa nyumba yake utatoweka; bidhaa zake zitamwagika mbali siku ya ghadhabu ya Mungu.
The increase of his house shall depart, flowing away in the day of his anger.
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu, urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye.”
This is the portion of the wicked man from God, and the heritage appointed to him by God.