< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
ויען איוב ויאמר
2 lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?
עד-אנה תוגיון נפשי ותדכאונני במלים
3 Mara kumi hivi mmenishutumu mimi; ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.
זה עשר פעמים תכלימוני לא-תבשו תהכרו-לי
4 Kama ni dhahiri kweli mimi nimekosa, makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.
ואף-אמנם שגיתי אתי תלין משוגתי
5 Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi,
אם-אמנם עלי תגדילו ותוכיחו עלי חרפתי
6 kisha ninyi mnapaswa kutambua kwamba Mungu amefanya mabaya kwangu mimi na amenikamata mimi katika mtego wake yeye.
דעו-אפו כי-אלוה עותני ומצודו עלי הקיף
7 Tazama, Mimi ninalia kwa sauti, “dhuluma!” lakini sipati jibu. Mimi ninaita kwa ajili ya msaada, lakini hakuna haki.
הן אצעק חמס ולא אענה אשוע ואין משפט
8 Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu.
ארחי גדר ולא אעבור ועל נתיבותי חשך ישים
9 Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu, na ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi.
כבודי מעלי הפשיט ויסר עטרת ראשי
10 Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande, na Mimi nimetoweka; yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.
יתצני סביב ואלך ויסע כעץ תקותי
11 Yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi; yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.
ויחר עלי אפו ויחשבני לו כצריו
12 Majeshi yake huja juu pamoja; wao wananikosesha tumaini kwa kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi wakizunguka hema yangu.
יחד יבאו גדודיו--ויסלו עלי דרכם ויחנו סביב לאהלי
13 Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi; watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi.
אחי מעלי הרחיק וידעי אך-זרו ממני
14 Vizazi vyangu vimeniangusha mimi; rafiki zangu wa karibu wamenisahamu mimi.
חדלו קרובי ומידעי שכחוני
15 Wale ambao mwanzoni walikaa kama wageni ndani ya nyumba yangu na watumishi wangu wa kike, hunihesabu mimi kama mgeni. Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao.
גרי ביתי ואמהתי לזר תחשבני נכרי הייתי בעיניהם
16 Mimi ninamwita mtumishi wangu, lakini yeye hanipi jibu japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.
לעבדי קראתי ולא יענה במו-פי אתחנן-לו
17 Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu; Hata mimi ninachukiwa na wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.
רוחי זרה לאשתי וחנתי לבני בטני
18 Hata watoto wachanga wananichukia mimi; ikiwa Mimi nitainuka kuzungumza, wao huzungumza dhidi yangu mimi.
גם-עוילים מאסו בי אקומה וידברו-בי
19 Rafiki zangu wote ninaowazoea wananichukia sana mimi; wale ambao Mimi ninawapenda wamegeuka kinyume na mimi.
תעבוני כל-מתי סודי וזה-אהבתי נהפכו-בי
20 Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu; Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.
בעורי ובבשרי דבקה עצמי ואתמלטה בעור שני
21 Iweni na huruma juu yangu mimi, muwe na huruma juu yangu mimi, rafiki zangu, kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mimi.
חנני חנני אתם רעי כי יד-אלוה נגעה בי
22 Kwa nini mnanitesa mimi kama ninyi mlikuwa Mungu? kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?
למה תרדפני כמו-אל ומבשרי לא תשבעו
23 Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini! Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
מי-יתן אפו ויכתבון מלי מי-יתן בספר ויחקו
24 Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!
בעט-ברזל ועפרת-- לעד בצור יחצבון
25 Lakini kama ilivyo kwangu mimi, Mimi ninafahamu kwamba mkombozi wangu anaishi, na kwamba hata mwisho atasimama katika nchi;
ואני ידעתי גאלי חי ואחרון על-עפר יקום
26 baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa, ndipo katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.
ואחר עורי נקפו-זאת ומבשרי אחזה אלוה
27 Mimi nitamwona yeye kwa macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine. Moyo wangu hushindwa ndani yangu mimi.
אשר אני אחזה-לי--ועיני ראו ולא-זר כלו כליתי בחקי
28 Kama mnatasema, 'Kwa jinsi gani tutamtesa yeye? Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;
כי תאמרו מה-נרדף-לו ושרש דבר נמצא-בי
29 ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga, kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga, hivyo kwamba wewe uweze kutambua kuna hukumu.”
גורו לכם מפני-חרב--כי-חמה עונות חרב למען תדעון שדין (שדון)

< Ayubu 19 >