< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
And he answered Job and he said.
2 lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?
Until when? will you torment! self my and will you crush? me with words.
3 Mara kumi hivi mmenishutumu mimi; ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.
This ten times you have insulted me not you have been ashamed you have ill-treated me.
4 Kama ni dhahiri kweli mimi nimekosa, makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.
And even truly I have erred with me it lodges error my.
5 Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi,
If truly above me you will magnify yourselves and you may argue on me disgrace my.
6 kisha ninyi mnapaswa kutambua kwamba Mungu amefanya mabaya kwangu mimi na amenikamata mimi katika mtego wake yeye.
Know then that God he has wronged me and net his over me he has closed.
7 Tazama, Mimi ninalia kwa sauti, “dhuluma!” lakini sipati jibu. Mimi ninaita kwa ajili ya msaada, lakini hakuna haki.
There! I cry out violence and not I am answered I cry for help and there not [is] justice.
8 Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu.
Way my he has walled up and not I will pass and on paths my darkness he puts.
9 Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu, na ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi.
Honor my from on me he has stripped off and he has removed [the] crown of head my.
10 Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande, na Mimi nimetoweka; yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.
He has torn down me all around and I have gone and he has uprooted like a tree hope my.
11 Yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi; yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.
And he has kindled towards me anger his and he has considered me himself like foes his.
12 Majeshi yake huja juu pamoja; wao wananikosesha tumaini kwa kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi wakizunguka hema yangu.
Together - they have come troops his and they have piled up on me way their and they have encamped all around tent my.
13 Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi; watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi.
Brothers my from with me he has put far away and acquaintances my surely they have become estranged from me.
14 Vizazi vyangu vimeniangusha mimi; rafiki zangu wa karibu wamenisahamu mimi.
They have ceased kindred my and acquaintances my they have forgotten me.
15 Wale ambao mwanzoni walikaa kama wageni ndani ya nyumba yangu na watumishi wangu wa kike, hunihesabu mimi kama mgeni. Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao.
[the] sojourners of House my and female servants my to a stranger they consider me a foreigner I have become in view their.
16 Mimi ninamwita mtumishi wangu, lakini yeye hanipi jibu japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.
To servant my I call and not he answers with mouth my I seek favor to him.
17 Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu; Hata mimi ninachukiwa na wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.
Breath my it is loathsome to wife my and I am repulsive to [the] sons of womb my.
18 Hata watoto wachanga wananichukia mimi; ikiwa Mimi nitainuka kuzungumza, wao huzungumza dhidi yangu mimi.
Also young boys they reject me I arise and they spoke against me.
19 Rafiki zangu wote ninaowazoea wananichukia sana mimi; wale ambao Mimi ninawapenda wamegeuka kinyume na mimi.
They abhor me all [the] men of council my and whom I love they have turned against me.
20 Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu; Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.
On skin my and on flesh my it clings bone my and I have escaped! with [the] skin of teeth my.
21 Iweni na huruma juu yangu mimi, muwe na huruma juu yangu mimi, rafiki zangu, kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mimi.
Show favor to me show favor to me O you friends my for [the] hand of God it has touched me.
22 Kwa nini mnanitesa mimi kama ninyi mlikuwa Mungu? kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?
Why? are you persecuting me like God and from flesh my not are you satisfied?
23 Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini! Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
Who? will he give then and they will be written down! words my who? will he give on the scroll so they may be inscribed.
24 Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!
With a stylus of iron and lead for ever in the rock they will be engraved!
25 Lakini kama ilivyo kwangu mimi, Mimi ninafahamu kwamba mkombozi wangu anaishi, na kwamba hata mwisho atasimama katika nchi;
And I I know vindicator my he lives and last on dust he will stand.
26 baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa, ndipo katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.
And after skin my people have struck off this and from flesh my I will see God.
27 Mimi nitamwona yeye kwa macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine. Moyo wangu hushindwa ndani yangu mimi.
Whom I - I will see for myself and own eyes my they will see and not a stranger they are faint kidneys my in bosom my.
28 Kama mnatasema, 'Kwa jinsi gani tutamtesa yeye? Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;
If you will say what? will we persecute him and [the] root of [the] matter it has been found in me.
29 ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga, kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga, hivyo kwamba wewe uweze kutambua kuna hukumu.”
Be afraid yourselves - of [the] sword for rage [is] iniquities of [the] sword so that you may know! (that a judgment. *Q(k)*)

< Ayubu 19 >