< Ayubu 18 >

1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Entonces Bildad el Suhita respondió,
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
“¿Hasta cuándo vas a buscar palabras? Considera, y después hablaremos.
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
Por qué se nos cuenta como animales, que se han vuelto inmundos a tus ojos?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
Tú que te desgarras en tu ira, ¿se abandonará la tierra por ti? ¿O la roca será removida de su lugar?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
“Sí, la luz de los impíos se apagará. La chispa de su fuego no brillará.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
La luz será oscura en su tienda. Su lámpara sobre él se apagará.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
Los pasos de su fuerza se acortarán. Su propio consejo le hará caer.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
Porque es arrojado a la red por sus propios pies, y se adentra en su malla.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
Una trampa lo tomará por el talón. Una trampa lo atrapará.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
Un lazo está escondido para él en la tierra, una trampa para él en el camino.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
Los terrores lo harán temer por todos lados, y le perseguirá los talones.
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
Su fuerza será famélica. Calamity estará listo a su lado.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
Los miembros de su cuerpo serán devorados. El primogénito de la muerte devorará sus miembros.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
Será desarraigado de la seguridad de su tienda. Será llevado ante el rey de los terrores.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
En su tienda habitará lo que no es suyo. El azufre será esparcido sobre su morada.
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
Sus raíces se secarán por debajo. Su rama será cortada por encima.
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
Su memoria perecerá de la tierra. No tendrá nombre en la calle.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
Será expulsado de la luz a las tinieblas, y expulsado del mundo.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
No tendrá ni hijo ni nieto en su pueblo, ni que queden restos en el lugar donde vivía.
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
Los que vengan después se asombrarán de su día, como los que fueron antes se asustaron.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
Ciertamente, tales son las moradas de los injustos. Este es el lugar del que no conoce a Dios”.

< Ayubu 18 >