< Ayubu 18 >

1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Et Baldad de Sauchée, dit:
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
Quand donc te reposeras-tu? contiens-toi, afin que nous parlions aussi.
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
Pourquoi devant toi sommes-nous muets comme des quadrupèdes?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
Tu te mets en colère. Qu'y a-t-il? Si tu meurs, la terre sous le ciel sera-t-elle inhabitée, et les montagnes s'écrouleront-elles jusqu'à la base?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
La lumière des impies s'éteindra, et d'eux il ne sortira point de flamme.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
La lumière est ténèbres en la demeure de l'impie; la lampe qui l'éclaire s'éteindra.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
Que les petits soient mis en possession de ses richesses; que ces conseils soient renversés.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
Son pied s'est pris au piège, que le filet l'enveloppe tout entier.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
Qu' il le retienne, et ceux qui ont soif de l'attaquer prendront courage.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
Le câble était caché en terre, il devait le heurter dans le chemin.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
Puissent les douleurs l'investir et le perdre, qu'elles l'entourent en foule à chacun de ses pas;
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
Qu'il sente les angoisses de la faim; une chute extraordinaire lui a été réservée.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
Que les doigts de ses pieds soient rongés; la mort dévorera de lui tout ce qu'elle trouvera mûr pour elle.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
Que la guérison fuie le toit qu'il habite, que la nécessité l'emprisonne comme s'il eût commis un crime contre le roi.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
Dans sa nuit fatale il se sera vainement abrité sous sa tente; tout ce qui fait sa gloire sera bouleversé par la foudre;
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
Au plus profond de la terre les racines de ses arbres sécheront; à la surface sa maison tombera.
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
Que tout souvenir de lui périsse sur la terre, et son nom appartiendra à la face invisible de l'univers.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
Qu'il soit chassé de la lumière pour entrer dans les ténèbres.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
Il sera inconnu à son peuple, et sa famille ne lui survivra pas sous la voûte du ciel. D'autres vivront des biens qu'il a eus;
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
à cause de lui finalement on gémira; d'abord on aura été frappé d'étonnement.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
Tel est le sort des pervers; ainsi s'écroule la maison de ceux qui ne connaissent pas le Seigneur.

< Ayubu 18 >