< Ayubu 18 >
1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Then answered Bildad the Shuchite, and said,
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
When will ye at length put an end to words? Come to an understanding, and afterward let us speak.
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
For what cause are we counted as beasts, reputed stupid your eyes?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
Thou, the one that teareth himself to pieces in his anger— shall for thy sake the earth be forsaken, and the rock be moved away out of its place?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
Ah, truly the light of the wicked will be quenched, and the spark of his fire shall not give light.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
The light becometh dark in his tent, and his lamp will be quenched above him.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
His powerful steps will be narrowed, and his own counsel will cast him down.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
For he is driven into the net by his own feet, and he taketh his walk upon a snare.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
The trap will seize him by the heel, and the robber will prevail over him.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
The cord is hidden for him in the ground, and a trap is set for him on the pathway.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
All around do terrors scare him, and chase him as he walketh along.
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
His first-born will suffer hunger, and calamity will be ready for his wife.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
It will devour the limbs of his body: yea, the first-born of death will devour his limbs.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
Then will be plucked up out of his tent his confidence, and [the evil] will urge him forward to the king of terrors.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
It will dwell in his tent, because it is no more his: there will be strewed sulphur on his habitation.
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
Beneath, his roots will be dried up, and above will his boughs he cut away.
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
His resemblance vanisheth from the earth, and no name remaineth for him in the streets.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
Men will thrust him out from light into darkness, and out of the world will they drive him.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
He will have neither son nor grandson among his people, nor any that escapeth in the places of his sojourning.
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
Because of his [calamitous] day are they that come after him astonished, and they that went before are seized with shuddering.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
Yea, such are the dwellings of the unjust, and this is the place of one that knew not God.