< Ayubu 18 >

1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Then answered Bildad the Shuhite, and said,
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
When will yee make an ende of your words? cause vs to vnderstande, and then wee will speake.
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
Wherefore are wee counted as beastes, and are vile in your sight?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
Thou art as one that teareth his soule in his anger. Shall the earth bee forsaken for thy sake? or the rocke remoued out of his place?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
Yea, the light of the wicked shalbe quenched, and the sparke of his fire shall not shine.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
The light shalbe darke in his dwelling, and his candle shalbe put out with him.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
The steps of his strength shalbe restrained, and his owne counsell shall cast him downe.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
For hee is taken in the net by his feete, and he walketh vpon the snares.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
The grenne shall take him by the heele, and the theefe shall come vpon him.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
A snare is layed for him in the ground, and a trappe for him in the way.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
Fearefulnesse shall make him afrayde on euery side, and shall driue him to his feete.
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
His strength shalbe famine: and destruction shalbe readie at his side.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
It shall deuoure the inner partes of his skinne, and the first borne of death shall deuoure his strength.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
His hope shalbe rooted out of his dwelling, and shall cause him to go to the King of feare.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
Feare shall dwell in his house (because it is not his) and brimstone shalbe scattered vpon his habitation.
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
His rootes shalbe dryed vp beneath, and aboue shall his branche be cut downe.
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
His remembrance shall perish from the earth, and he shall haue no name in the streete.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
They shall driue him out of the light vnto darkenesse, and chase him out of the world.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
Hee shall neither haue sonne nor nephewe among his people, nor any posteritie in his dwellings.
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
The posteritie shalbe astonied at his day, and feare shall come vpon the ancient.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
Surely such are the habitations of the wicked, and this is the place of him that knoweth not God.

< Ayubu 18 >