< Ayubu 18 >

1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Then Bildad the Shuhite spoke up and said,
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
“How long will you go on talking, hunting for the right words to say? Talk sense if you want us to reply!
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
Do you think we're dumb animals? Do we look stupid to you?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
You tear yourself apart with your anger. Do you think the earth has to be abandoned, or the mountains moved, just because of you?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
It's certain that the life of the wicked will end like a lamp that is snuffed out—their flame will shine no more.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
The light in their home goes out, the lamp hanging above is extinguished.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
Instead of taking strong strides they stumble, and their own plans cause them to fall.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
Their own feet trip them up and they are caught in a net; as they walk along they fall into a pit.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
A trap grabs them by the heel; a snare tightens around them.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
A noose is hidden on the ground for them; a rope is stretched across the path to trip them.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
Terrors scare the wicked, coming at them from every side, chasing them, biting at their heels.
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
Hunger robs them of strength; disaster waits for them when they fall.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
Disease devours their skin; deadly disease consumes their limbs.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
They are torn from the homes they trusted in and taken to the king of terrors.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
People they don't know will live in their homes; sulfur will be scattered where they used to live.
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
They wither away, roots below and branches above;
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
the memory of them fades from the earth; nobody remembers their names any more.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
They are thrown out of light into darkness, driven from the world.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
They have no children or descendants among their people, and no survivors where they used to live.
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
People of the west are appalled at what happens to them. People of the east are shocked.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
This is what happens to the homes of the wicked, to the places of those who reject God.”

< Ayubu 18 >