< Ayubu 17 >

1 Roho yangu imemezwa, na siku zangu zimekwisha; kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.
Mi alma se agota, mis días se extinguen. El sepulcro está preparado para mí.
2 Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami; ni lazima daima jicho langu litazame kukasirisha kwao.
No hay conmigo sino burladores, y mis ojos se fijan en su provocación.
3 Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe; nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?
Te ruego, deposita una fianza ante Ti mismo. ¿Quién quiere ser mi garante?
4 Kwa kuwa wewe Mungu umemeitunza mioyo yao kutoka katika ufahamu; kwa hiyo, wewe hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.
Porque cerraste su corazón al entendimiento. Por tanto, no los exaltarás.
5 Yeye ambaye huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
Al que traiciona a sus amigos por recompensa, les desfallecerán los ojos a sus hijos.
6 Lakini amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu; wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.
Pero Él me convirtió en un refrán de la gente. Soy uno a quien los hombres escupen.
7 Jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni; sehemu zangu zote za mwili ni nyembamba kama vivuli.
Mis ojos se oscurecieron por la angustia, y todos mis miembros son como una sombra.
8 Watu wanyoofu watapendezwa na hiki; mtu asiye na hatia atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi ya watu wasiomcha Mungu.
Los rectos se asombran de esto, y el inocente se levanta contra el impío.
9 Mtu mwenye haki ataendelea katika njia yake; yeye ambaye ana mikono iliyo safi ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi.
Sin embargo, el justo se aferra a su camino, y el limpio de manos aumentará sus fuerzas.
10 Lakini kama ilivyo kwenu ninyi nyote, njooni sasa; Mimi sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu ninyi.
Pero ahora, vuelvan todos ustedes y vengan acá. Pero entre ustedes no hallaré algún sabio.
11 Siku zangu zimepita; mipango yangu imenyamazishwa na hivyo ni matumaini ya moyo wangu.
Mis días pasaron. Mis planes se deshicieron, aun los anhelos de mi corazón
12 Watu hawa, wenye kukejeli, badili usiku kuwa mchana; mchana uko karibu kuwa giza.
que solían cambiar la noche en día. La luz está después de la oscuridad.
13 Tangu mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu; tangu Mimi nimetandaza kiti changu katika giza; (Sheol h7585)
Si espero, yo sé que el Seol es mi habitación. En la tenebrosidad tengo extendida mi cama. (Sheol h7585)
14 tangu Mimi nimesema na shimo 'Wewe ni baba yangu,' na kwa funza, 'Wewe ni mama yangu au dada yangu;
A la descomposición digo: ¡Padre mío! Y al gusano: ¡Madre mía, hermana mía!
15 liko wapi tena tumaini langu? Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?
¿Dónde está entonces mi esperanza? ¿Quién verá mi bien?
16 Tumaini litakwenda pamoja na mimi katika milango ya Kuzimu wakati sisi tutakapokwenda katika mavumbi? (Sheol h7585)
Descenderá conmigo al Seol y juntos bajaremos al polvo. (Sheol h7585)

< Ayubu 17 >