< Ayubu 17 >

1 Roho yangu imemezwa, na siku zangu zimekwisha; kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.
My spirit is consumed, my days are extinct, The grave is [ready] for me.
2 Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami; ni lazima daima jicho langu litazame kukasirisha kwao.
Surely there are mockers with me, And mine eye dwelleth upon their provocation.
3 Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe; nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?
Give now a pledge, be surety for me with thyself; Who is there that will strike hands with me?
4 Kwa kuwa wewe Mungu umemeitunza mioyo yao kutoka katika ufahamu; kwa hiyo, wewe hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.
For thou hast hid their heart from understanding: Therefore shalt thou not exalt [them].
5 Yeye ambaye huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
He that denounceth his friends for a prey, Even the eyes of his children shall fail.
6 Lakini amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu; wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.
But he hath made me a byword of the people; And they spit in my face.
7 Jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni; sehemu zangu zote za mwili ni nyembamba kama vivuli.
Mine eye also is dim by reason of sorrow, And all my members are as a shadow.
8 Watu wanyoofu watapendezwa na hiki; mtu asiye na hatia atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi ya watu wasiomcha Mungu.
Upright men shall be astonished at this, And the innocent shall stir up himself against the godless.
9 Mtu mwenye haki ataendelea katika njia yake; yeye ambaye ana mikono iliyo safi ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi.
Yet shall the righteous hold on his way, And he that hath clean hands shall wax stronger and stronger.
10 Lakini kama ilivyo kwenu ninyi nyote, njooni sasa; Mimi sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu ninyi.
But as for you all, come on now again; And I shall not find a wise man among you.
11 Siku zangu zimepita; mipango yangu imenyamazishwa na hivyo ni matumaini ya moyo wangu.
My days are past, my purposes are broken off, Even the thoughts of my heart.
12 Watu hawa, wenye kukejeli, badili usiku kuwa mchana; mchana uko karibu kuwa giza.
They change the night into day: The light, [say they], is near unto the darkness.
13 Tangu mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu; tangu Mimi nimetandaza kiti changu katika giza; (Sheol h7585)
If I look for Sheol as my house; If I have spread my couch in the darkness; (Sheol h7585)
14 tangu Mimi nimesema na shimo 'Wewe ni baba yangu,' na kwa funza, 'Wewe ni mama yangu au dada yangu;
If I have said to corruption, Thou art my father; To the worm, [Thou art] my mother, and my sister;
15 liko wapi tena tumaini langu? Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?
Where then is my hope? And as for my hope, who shall see it?
16 Tumaini litakwenda pamoja na mimi katika milango ya Kuzimu wakati sisi tutakapokwenda katika mavumbi? (Sheol h7585)
It shall go down to the bars of Sheol, When once there is rest in the dust. (Sheol h7585)

< Ayubu 17 >