< Ayubu 16 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
ויען איוב ויאמר
2 “Mimi nimevisikia vitu hivyo vingi; ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.
שמעתי כאלה רבות מנחמי עמל כלכם
3 Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho? Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?
הקץ לדברי-רוח או מה-ימריצך כי תענה
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi mnavyofanya, kama ninyi mngekuwa katika nafasi yangu; Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja dhidi yenu na kutikisa kichwa changu kwenu ninyi katika dhihaka.
גם אנכי-- ככם אדברה לו יש נפשכם תחת נפשי-- אחבירה עליכם במלים ואניעה עליכם במו ראשי
5 Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!
אאמצכם במו-פי וניד שפתי יחשך
6 Ikiwa Mimi ninazungumza, kuomboleza kwangu hakujasikilizwa; Ikiwa nikiendelea katika kuzungumza, jinsi gani mimi ninaidiwa?
אם-אדברה לא-יחשך כאבי ואחדלה מה-מני יהלך
7 Lakini sasa, Mungu,
אך-עתה הלאני השמות כל-עדתי
8 wewe umenifanya mimi kuchoka; wewe umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa. Wewe umenifanya mimi kukauka, ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi; kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi ya macho yangu.
ותקמטני לעד היה ויקם בי כחשי בפני יענה
9 Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.
אפו טרף וישטמני--חרק עלי בשניו צרי ילטש עיניו לי
10 Watu wameachama na midomo iliyowazi juu yangu; wamenipiga mimi katika shavu kwa kunitukana; wamekusanyika pamoja kinyume changu mimi.
פערו עלי בפיהם--בחרפה הכו לחיי יחד עלי יתמלאון
11 Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu.
יסגירני אל אל עויל ועל-ידי רשעים ירטני
12 Mimi nilikuwa katika wepesi, na yeye amenivunjavunja mimi vipande. Hakika, amenichukua mimi kwa shingo na ameniponda mimi vipande vipande; yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.
שלו הייתי ויפרפרני-- ואחז בערפי ויפצפצני ויקימני לו למטרה
13 Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi; Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi.
יסבו עלי רביו-- יפלח כליותי ולא יחמל ישפך לארץ מררתי
14 yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta wangu tena na tena; yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.
יפרצני פרץ על-פני-פרץ ירץ עלי כגבור
15 nguo ya magunia juu ya ngozi yangu; Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.
שק תפרתי עלי גלדי ועללתי בעפר קרני
16 Uso wangu ni mwekundu na kuomboleza; juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti
פני חמרמרה (חמרמרו) מני-בכי ועל עפעפי צלמות
17 ingawa hakuna dhuluma katika mikono yangu, na kuomba kwangu ni safi.
על לא-חמס בכפי ותפלתי זכה
18 Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi; acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.
ארץ אל-תכסי דמי ואל-יהי מקום לזעקתי
19 Hata sasa, tazama, ushuhuda wangu uko mbinguni; yeye ambaye ashuhudiaye kwa ajili yangu mimi yuko juu.
גם-עתה הנה-בשמים עדי ושהדי במרמים
20 Rafiki zangu wananicheka kwa dharau, lakini jicho langu linamwaga machozi kwa Mungu.
מליצי רעי אל-אלוה דלפה עיני
21 Mimi ninaomba ule ushuhuda ulioko mbinguni kumtetea mtu huyu na Mungu kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.
ויוכח לגבר עם-אלוה ובן-אדם לרעהו
22 Kwa maana wakati miaka michache itakapokuwa imepita, Mimi nitakwenda mahali ambapo mimi sitaweza kurudi.
כי-שנות מספר יאתיו וארח לא-אשוב אהלך

< Ayubu 16 >