< Ayubu 16 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said,
2 “Mimi nimevisikia vitu hivyo vingi; ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.
I have heard many such things: miserable comforters [are] ye all.
3 Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho? Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?
Shall vain words have an end? or what emboldeneth thee that thou answerest?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi mnavyofanya, kama ninyi mngekuwa katika nafasi yangu; Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja dhidi yenu na kutikisa kichwa changu kwenu ninyi katika dhihaka.
I also could speak as ye [do]: if your soul were in my soul's stead, I could heap up words against you, and shake my head at you.
5 Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!
[But] I would strengthen you with my mouth and the moving of my lips should assuage [your grief].
6 Ikiwa Mimi ninazungumza, kuomboleza kwangu hakujasikilizwa; Ikiwa nikiendelea katika kuzungumza, jinsi gani mimi ninaidiwa?
Though I speak, my grief is not assuaged: and [though] I forbear, what am I eased?
7 Lakini sasa, Mungu,
But now he hath made me weary: thou hast made desolate all my company.
8 wewe umenifanya mimi kuchoka; wewe umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa. Wewe umenifanya mimi kukauka, ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi; kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi ya macho yangu.
And thou hast filled me with wrinkles, [which] is a witness [against me]: and my leanness rising up in me beareth witness to my face.
9 Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.
He teareth [me] in his wrath, who hateth me: he gnasheth upon me with his teeth; my enemy sharpeneth his eyes upon me.
10 Watu wameachama na midomo iliyowazi juu yangu; wamenipiga mimi katika shavu kwa kunitukana; wamekusanyika pamoja kinyume changu mimi.
They have gaped upon me with their mouth; they have smitten me upon the cheek reproachfully; they have gathered themselves against me.
11 Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu.
God hath delivered me to the ungodly, and turned me over into the hands of the wicked.
12 Mimi nilikuwa katika wepesi, na yeye amenivunjavunja mimi vipande. Hakika, amenichukua mimi kwa shingo na ameniponda mimi vipande vipande; yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.
I was at ease, but he hath broken me asunder: he hath also taken [me] by my neck, and shaken me to pieces, and set me up for his mark.
13 Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi; Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi.
His archers encompass me; he cleaveth my reins asunder, and doth not spare; he poureth out my gall upon the ground.
14 yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta wangu tena na tena; yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.
He breaketh me with breach upon breach, he runneth upon me like a giant.
15 nguo ya magunia juu ya ngozi yangu; Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.
I have sewed sackcloth upon my skin, and defiled my horn in the dust.
16 Uso wangu ni mwekundu na kuomboleza; juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti
My face is foul with weeping, and on my eyelids [are] the shades of death;
17 ingawa hakuna dhuluma katika mikono yangu, na kuomba kwangu ni safi.
Not for [any] injustice in my hands: also my prayer [is] pure.
18 Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi; acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.
O earth, cover not thou my blood, and let my cry have no place.
19 Hata sasa, tazama, ushuhuda wangu uko mbinguni; yeye ambaye ashuhudiaye kwa ajili yangu mimi yuko juu.
Also now, behold, my witness [is] in heaven, and my record [is] on high.
20 Rafiki zangu wananicheka kwa dharau, lakini jicho langu linamwaga machozi kwa Mungu.
My friends scorn me: [but] my eye poureth out [tears] to God.
21 Mimi ninaomba ule ushuhuda ulioko mbinguni kumtetea mtu huyu na Mungu kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.
O that one might plead for a man with God, as a man [pleadeth] for his neighbor!
22 Kwa maana wakati miaka michache itakapokuwa imepita, Mimi nitakwenda mahali ambapo mimi sitaweza kurudi.
When a few years are come, then I shall go the way [whence] I shall not return.

< Ayubu 16 >