< Ayubu 16 >
1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
And Job answered and said,
2 “Mimi nimevisikia vitu hivyo vingi; ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.
I have heard many such things: grievous comforters are ye all.
3 Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho? Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?
Shall words of wind have an end? or what provoketh thee that thou answerest?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi mnavyofanya, kama ninyi mngekuwa katika nafasi yangu; Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja dhidi yenu na kutikisa kichwa changu kwenu ninyi katika dhihaka.
I also could speak as ye: if your soul were in my soul's stead, I could join together words against you, and shake my head at you;
5 Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!
[But] I would encourage you with my mouth, and the solace of my lips should assuage [your pain].
6 Ikiwa Mimi ninazungumza, kuomboleza kwangu hakujasikilizwa; Ikiwa nikiendelea katika kuzungumza, jinsi gani mimi ninaidiwa?
If I speak, my pain is not assuaged; and if I forbear, what am I eased?
But now he hath made me weary; ...thou hast made desolate all my family;
8 wewe umenifanya mimi kuchoka; wewe umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa. Wewe umenifanya mimi kukauka, ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi; kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi ya macho yangu.
Thou hast shrivelled me up! it is become a witness; and my leanness riseth up against me, it beareth witness to my face.
9 Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.
His anger teareth and pursueth me; he gnasheth with his teeth against me; [as] mine adversary he sharpeneth his eyes at me.
10 Watu wameachama na midomo iliyowazi juu yangu; wamenipiga mimi katika shavu kwa kunitukana; wamekusanyika pamoja kinyume changu mimi.
They gape upon me with their mouth; they smite my cheeks reproachfully; they range themselves together against me.
11 Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu.
God hath delivered me over to the iniquitous man, and hurled me into the hands of the wicked.
12 Mimi nilikuwa katika wepesi, na yeye amenivunjavunja mimi vipande. Hakika, amenichukua mimi kwa shingo na ameniponda mimi vipande vipande; yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.
I was at rest, but he hath shattered me; he hath taken me by the neck and shaken me to pieces, and set me up for his mark.
13 Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi; Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi.
His arrows encompass me round about, he cleaveth my reins asunder and doth not spare; he poureth out my gall upon the ground.
14 yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta wangu tena na tena; yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.
He breaketh me with breach upon breach; he runneth upon me like a mighty man.
15 nguo ya magunia juu ya ngozi yangu; Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.
I have sewed sackcloth upon my skin, and rolled my horn in the dust.
16 Uso wangu ni mwekundu na kuomboleza; juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti
My face is red with weeping, and on my eyelids is the shadow of death;
17 ingawa hakuna dhuluma katika mikono yangu, na kuomba kwangu ni safi.
Although there is no violence in my hands, and my prayer is pure.
18 Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi; acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.
O earth, cover not my blood, and let there be no place for my cry!
19 Hata sasa, tazama, ushuhuda wangu uko mbinguni; yeye ambaye ashuhudiaye kwa ajili yangu mimi yuko juu.
Even now, behold, my Witness is in the heavens, and he that voucheth for me is in the heights.
20 Rafiki zangu wananicheka kwa dharau, lakini jicho langu linamwaga machozi kwa Mungu.
My friends are my mockers; mine eye poureth out tears unto God.
21 Mimi ninaomba ule ushuhuda ulioko mbinguni kumtetea mtu huyu na Mungu kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.
Oh that there were arbitration for a man with God, as a son of man for his friend!
22 Kwa maana wakati miaka michache itakapokuwa imepita, Mimi nitakwenda mahali ambapo mimi sitaweza kurudi.
For years [few] in number shall pass, — and I shall go the way [whence] I shall not return.