< Ayubu 15 >

1 Ndipo Elifazi Mtemani alijibu na kusema,
ויען אליפז התימני ויאמר׃
2 Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?
החכם יענה דעת רוח וימלא קדים בטנו׃
3 Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?
הוכח בדבר לא יסכון ומלים לא יועיל בם׃
4 Dhahiri, wewe wafifisha heshima ya Mungu; Wewe wazuia heshima kwa yeye,
אף אתה תפר יראה ותגרע שיחה לפני אל׃
5 kwa maana uovu wako hufundisha midomo yako; Wewe wachagua kuwa na ulimi wa mtu mwenye hila.
כי יאלף עונך פיך ותבחר לשון ערומים׃
6 Mdomo wako mwenyewe hukukukumu wewe, siyo wangu; hakika, midomo yako mwenyewe hushuhudia dhidi yako wewe.
ירשיעך פיך ולא אני ושפתיך יענו בך׃
7 Je, wewe ni mwanadamu wa kwanza ambaye aliyezaliwa? Wewe ulikuwepo kabla ya vilima kuwepo?
הראישון אדם תולד ולפני גבעות חוללת׃
8 Wewe Umewahi kusikia maarifa ya siri ya Mungu? Je, wewe wajihesabia mwenye hekima wewe mwenyewe?
הבסוד אלוה תשמע ותגרע אליך חכמה׃
9 Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho sisi hatukijui? Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho hakiko katika sisi?
מה ידעת ולא נדע תבין ולא עמנו הוא׃
10 Pamoja nasi wapo pia wenye mvi na watu wazee sana ambao ni wazee zaidi kuliko baba yako.
גם שב גם ישיש בנו כביר מאביך ימים׃
11 Je, faraja ya Mungu ni ndogo sana kwako, maneno ambayo ni ya upole dhidi yako wewe?
המעט ממך תנחמות אל ודבר לאט עמך׃
12 Kwa nini moyo wako wewe unakupeleka mbali? Kwa nini macho yako yananga'ra,
מה יקחך לבך ומה ירזמון עיניך׃
13 ili ya kwamba kuirejesha roho yako kwa Mungu na kuyatoa maneno hayo kutoka katika mdomo wako?
כי תשיב אל אל רוחך והצאת מפיך מלין׃
14 Je, mwanadamu yeye ni nini kwamba yeye anapaswa kuwa safi? Yeye mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ni nini kwamba yeye anapaswa awe mwenye haki?
מה אנוש כי יזכה וכי יצדק ילוד אשה׃
15 Tazama, Mungu haweki tumaini lake hata kwa mmoja wake aliye mtakatifu; Hakika, mbingu haziko safi machoni pake yeye;
הן בקדשו לא יאמין ושמים לא זכו בעיניו׃
16 jinsi gani asivyo safi ni mmoja aliye mbaya na mla rushwa, mtu ambaye hunywa uovu kama maji!
אף כי נתעב ונאלח איש שתה כמים עולה׃
17 Mimi nitakuonyesha wewe; Nisikilize mimi; Mimi nitakutangazia wewe vitu ambavyo nimeviona,
אחוך שמע לי וזה חזיתי ואספרה׃
18 vitu ambavyo watu wenye hekima wamepita chini yake kutoka kwa baba zao, vile vitu ambavyo mababu zao hawakuvificha.
אשר חכמים יגידו ולא כחדו מאבותם׃
19 Hawa walikuwa mababu zao, ambao kwao pekee nchi walipewa, na miongoni mwao hakuna mgeni aliyepita.
להם לבדם נתנה הארץ ולא עבר זר בתוכם׃
20 Mtu mwovu hupitia katika maumivu siku zake zote, idadi ya miaka iliyowekwa juu kwa mtesaji kuteseka.
כל ימי רשע הוא מתחולל ומספר שנים נצפנו לעריץ׃
21 Sauti ya vitisho katika masikio yake; pindi yeye yuko katika kufanikiwa, mharibu atakuja juu yake yeye.
קול פחדים באזניו בשלום שודד יבואנו׃
22 Yeye hafikiri kwamba yeye atarudi kutoka katika giza; Upanga humngojea yeye.
לא יאמין שוב מני חשך וצפו הוא אלי חרב׃
23 Yeye huenda sehemu mbali mbali kwa ajili ya mkate, akisema, 'Kiko wapi? ' Yeye anatambua kuwa siku ya giza iko mkononi.
נדד הוא ללחם איה ידע כי נכון בידו יום חשך׃
24 Dhiki na mateso makali humfanya aogope; wao hushinda dhidi yake yeye, kama mfalme tayari kwa vita.
יבעתהו צר ומצוקה תתקפהו כמלך עתיד לכידור׃
25 Kwa sababu yeye ameunyosha mkono wake dhidi ya Mungu na ameishi kwa kiburi dhidi ya aliye mkuu,
כי נטה אל אל ידו ואל שדי יתגבר׃
26 huyu mtu mwovu hukimbia kwa Mungu na shingo ngumu, kwa vifundo vikubwa vya ngao.
ירוץ אליו בצואר בעבי גבי מגניו׃
27 Hii ni kweli, hata ingawa yeye amefunika uso wake kwa mafuta yake na amekusanya mafuta juu ya viuno vyake,
כי כסה פניו בחלבו ויעש פימה עלי כסל׃
28 na ameishi katika miji yenye ukiwa; katika nyumba ambazo hakuna mwanadamu anayeishi humo sasa na ambazo zilikuwa tayari kuwa magofu.
וישכון ערים נכחדות בתים לא ישבו למו אשר התעתדו לגלים׃
29 Yeye hatakuwa tajiri; utajiri wake yeye hautadumu; hata kivuli chake hakitadumu katika nchi.
לא יעשר ולא יקום חילו ולא יטה לארץ מנלם׃
30 Yeye hatatoka nje ya giza; mwali wa moto utakausha matawi yake; katika pumzi ya kinywa cha Mungu yeye ataenda zake.
לא יסור מני חשך ינקתו תיבש שלהבת ויסור ברוח פיו׃
31 Mwacheni yeye asitumaini katika vitu visivyofanya kazi, akijidanganya yeye mwenyewe; maana upuuzi utakuwa mshahara wake yeye.
אל יאמן בשו נתעה כי שוא תהיה תמורתו׃
32 Itatokea kabla ya wakati wake yeye atapaswa kufa; tawi lake halitakuwa kijani.
בלא יומו תמלא וכפתו לא רעננה׃
33 Yeye atazipukutisha zabibu zake zisizovunwa kama mzabibu; yeye atayaondoa maua yake kama mti wa mzeituni.
יחמס כגפן בסרו וישלך כזית נצתו׃
34 Kwa maana msaada wa watu wasiomcha Mungu utakuwa tasa; moto utateketeza hema za rushwa.
כי עדת חנף גלמוד ואש אכלה אהלי שחד׃
35 Wao wanabeba mimba yenye ubaya na kuzaa uovu; tumbo lao hutunga mimba ya udanganifu.
הרה עמל וילד און ובטנם תכין מרמה׃

< Ayubu 15 >